Mkuu
wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John
Mongella akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa
Tanzania Bara itakayofanyika Jijini Mwanza,
maadhimisho hayo yanafanyika Mkoani humo kwa mara ya kwanza.
Sehemu ya Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.
John Mongella na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa
Tanzania Bara yatakayofanyika Jijini Mwanza, maadhimisho hayo yanafanyika mkoani humo kwa mara ya kwanza.
Na
Mwandishi Wetu- Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi
katika maadhimisho ya sherehe za miaka 58 ya Uhuru wa Tanzania Bara na miaka 57
ya Jamhuri zinazotarajiwa kufanyika
Kitaifa mkoani Mwanza.
Akizungumza na waandishi
wa habari Mkuu wa Mkoa huo Mhe. John Mongella amesema kuwa maadhimisho hayo
yatafanyika Disemba 9, 2019 kwa mara ya kwanza katika mkoa huo katika uwanja wa
CCM Kirumba.
Kauli mbiu ya sherehe
hizo ni “ Miaka 58 ya Uhuru na miaka57 ya Jamhuri:Uzalendo, Uwajibikaji na
Ubunifu ni Msingi wa Ujenzi wa Uchumi wa Taifa Letu,” Alisistiza Mhe. Mongella.
Akifafanua amesema
kuwa Shughuli zitakazofanyika wakati wa madhimisho hayo ni pamoja na gwaride
maalum, burudani kutoka kwa wasanii wa kizazi kipya,ngoma za asili kutoka mikoa
ya Mwanza, Kagera na Mara.
Aidha Mhe. Mongella
amesema kuwa kutakuwa na shughuli mbalimbali kuelekea maadhimisho hayo ikiwemo
Mashindano ya ngonjera, Maigizo,Kwaya,Mashairi, Mashindano ya mbio za
mitumbwi,Bonanza la michezo, mchezo wa bao, na mechi ya mpira wa miguu.
Shughuli za kikanda
zitakazofanyika ni pamoja Kongamano la
Wanafunzi wa vyuo vya Elimu ya Juu litakalofanyika tarehe 6, Disemba, 2019 Chuo
Kikuu cha Mtakatifu Augustino Mwanza.
Alibainisha kuwa
baadhi ya viongozi wanaotarajiwa kuhudhuria sherehe hizo ni pamoja na Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,Waziri mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa na Rais wa Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe Dkt. Ali Mohamed
Shein.
Viongozi wastaafu
wakiwemo Marais, Makamu wa Rais na Mawaziri Wakuu ni miongoni mwa waalikwa wa
sherehe hizo,Aidha , Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Taasisi mbalimbali za
Serikali na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini ni miongoni mwa waalikwa wa
sherehe hizo.
Juma la kilele cha
maadhimisho hayo litakuwa na shughuli mbalimbali zitakazofanyika kikanda
kuanzia Disemba 2, 2019 hadi tarehe 8 Disemba, 2019 kwenye mikoa ya Kagera,
Mara, Geita, Simiyu, Shinyanga na Mwanza.
No comments:
Post a Comment