Mwezeshaji wa Kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Benezeth Lutege akifafanua namna ya kufanya Tathmini ya vimelea hatarishi vya magonjwa kwa kutumia Dhana ya Afya moja wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa sekta za afya na wadau wa Afya moja kutoka ngazi za Halmashauri mkoani Arusha, tarehe 22 Novemba , 2019.
KWA mara ya kwanza Barani Afrika, Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kufanya mafunzo
katika ngazi ya mkoa na Halmashauri kwa kutumia dhana ya Afya moja kuwajengea uwezo
wadau wa Afya moja juu ya namna ya kufanya tathmini ya vimelea hatarishi vya magonjwa.
Mafunzo hayo yamewakutanisha wadau wa Afya moja na wataalam kutoka sekta za afya ya
binadamu, wanyama pori, mifugo, kilimo na mazingira. Wadau hao na wataalam kutoka
sekta hizo za afya wamepata mafunzo ya namna ya kufanya tathmini hiyo kwa magonjwa ya
Kichaa cha mbwa, Kimeta na Ugonjwa wa Brusela (Ugonjwa wa Kutupa mimba kwa
wanyama).
Kufuatia nchi ya Tanzania kuwa imepiga hatua katika uratibu wa masuala ya Afya moja,
ambayo ni dhana inayojumuisha sekta ya afya ya binadamu, wanyamapori, mifugo, kilimo
na mazingira katika kujiandaa, kufuatilia na kukabili magonjwa yanayoathiri binadamu.
Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Dawati la Uratibu wa Afya moja kwa kushirikiana na Shirika la
Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) imeratibu mafunzo hayo yaliyotolewa na
wakufunzi wa hapa nchini waliojengewa uwezo na wataalamu kutoka Makao makuu
ya Shirika la Afya Duniani (WHO), Makao makuu ya Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja
wa Mataifa (FAO), pamoja na Shirika linaloshughulika na Afya ya Wanyama (OIE).
Akiongea wakati wa kufunga mafunzo hayo tarehe 22 Novemba 2019,Jijini Arusha, Mkurugenzi wa Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe, amebainisha kuwa ushirikiano wa wadau wa Afya moja na wataalam na sekta za Afya kwa kutumia dhana ya Afya Moja hivi sasa ni agenda ya dunia nzima. Aidha amefafanua kuwa dhana hiyo inapunguza gharama katika kushughulikia tishio la magonjwa yanayotokana na vimelea vyenye uwezo wa kutoka kwa wanyama na kwenda kwa binadamu na hata mimea (mazingira) na kusababisha magonjwa na hata usugu wa vimelea vya magonjwa.
“Wadau wa afya moja wanawajibika kupanga mikakati mbalimbali ya udhibiti, ulinzi na
usalama katika kuzuia, kujiandaa na kukabali magonjwa ambukizi. Moja ya mkakati
ulioibuliwa Kitaifa na kimataifa ni kujiandaa kwa kuwafundisha wataalam wa sekta
mbalimbali za afya jinsi ya kufanya tathmini ya hatari ya vimelea vya magonjwa ambukizi
kwa ushirikiano.” Amesema . Kanali Matamwe.
Kwa upande wake, Mwezeshaji wa Mafunzo hayo kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la
Umoja wa Mataifa (FAO), Tanzania, Bi. Niwael Mtui amefafanua kuwa Shirika hilo moja ya
kipaumbele chake ni kupunguza umasikini na kuongeza kipato cha wananchi, hivyo Shirika
hilo linashirikiana na serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, katika kujenga
uwezo wa ndani ya nchi kwa kuwafundisha wataalam wa sekta za Afya katika kudhibiti
magonjwa ambapo uwezo huo utasaidia kuimarisha afya ya binadamu na mifugo na
hatimaye kipato kitaongezeka na umasikini utapungua
Wakiongea kwa nyakati tofauti washiriki wa mafunzo hayo wamebainisha kuwa wamekuwa wakifanya tathmini za vimelela hatarishi vya magonjwa hapa nchini lakini tathmini hizo zimekuwa ni za kisekta kwani hazikuwa zinazingatia ushirikiano kwa maana ya dhana ya Afya moja. Aidha walifafanua kuwa mafunzo hayo yamewajengea uwezo wa kutumia Dhana ya Afya moja kwa kuwa inapunguza gharama katika kushughulikia tishio la magonjwa yanayotokana na vimelea vyenye uwezo wa kutoka kwa wanyama na kwenda kwa binadamu na hata mimea (mazingira) na kusababisha magonjwa na hata usugu wa vimelea vya magonjwa.
Tarehe 13 Februari 2018, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Kassim Majaliwa alizindua Dawati la Uratibu la Afya moja chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu,
likiwa na lengo la kusimamia na kuratibu shughuli za Afya moja nchini.
Kwa kutambua umuhimu huo Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, kupitia Dawati
la Uratibu wa Afya moja kwa kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa
Mataifa (FAO) na wadau waliandaa na kuratibu mafuzo hayo, ambapo wataalamu wa sekta
za Afya na Wadau wa Afya moja kutoka Halmashauri nne za mkoa
wa Arusha (Halmasahauri ya Arusha, Monduli, Ngorongoro na Karatu) walishirki mafunzo
hayo
No comments:
Post a Comment