Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza akifungua tamasha
la michezo la wiki ya kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyo ambukiza leo jijini
Dodoma ambapo kilele chake ni Novemba 14, 2019 ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa
kuwa Waziri Mkuu wa Jahuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Mjaliwa.
Na
Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma
Waajiri
wametakiwa kuboresha mazingira ya kazi kwa kuhakikisha watumishi wanashiriki
katika michezo na kufanya mazoezi
maeneo yao ya kazi.
Rai
hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Juliana
Shonza leo wakati wa ufunguzi wa tamasha la michezo la wiki ya kuzuia na
kudhibiti magonjwa yasiyo ambukiza linalofanyika katika uwanja wa Jamhuri
jijini Dodoma ambapo kilele chake ni Novemba 14, 2019 ambapo Mgeni Rasmi
anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jahuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Mjaliwa.
“Mnaweza kuanzisha timu
mbalimbali za michezo
na kutenga siku maalum katika mwezi kwa ajili ya
mabonanza ya michezo kwa kuweka mazingira rafiki
ya kufanyia mazoezi kazini kwa kununua vifaa na kutenga
vyumba vya mazoezi. Hii itaimarisha afya za watumishi na kupunguza gharama za matibabu
katika taasisi husika.” Naibu Waziri Juliana Shonza.
Naibu
Waziri Shonza amesema kuwa tamasha hilo linalenga kuhamasisha wananchi kushiriki
katika michezo mbalimbali na mazoezi ya viungo ili kukabiliana na magonjwa
yasiyoambukiza ambayo yamekuwa yakiongezeka hapa nchini.
Magonjwa
yasioyoambukiza hutokana na mitindo
isiyofaa ya maisha kama matumizi ya
tumbaku, lishe duni, matumizi ya pombe kupita kiasi, pamoja na kutoshughulisha
mwili au kutofanya mazoezi ya viungo mara kwa mara.
Magonjwa
hayo ni kisukari, shinikizo la juu la damu, magonjwa ya
moyo na mishipa,
saratani, pumu na magonjwa ya akili ambayo yamekuwa sugu na yana gharama
kubwa za matibabu ambapo amesema kuwa watu
wengi hufikiria mazoezi ni lazima
ukimbie au ucheze mpira, la
hasha.Mazoezi ni jambo lolote linalohusisha misuli na kusababisha kuongezeka
kwa mapigo ya
moyo na kasi
ya kupumua.
Wataalam
wa afya wanasema kuwa kiwango cha
mazoezi kinacholeta faida
ni mazoezi yasiyopungua dakika 30
kwa siku angalau siku tatu kwa wiki
na yanayomfanya mtu kutokwa
na jasho.
Aidha,
Naibu Waziri amesisitiza kuwa kupitia tamasha hilo, ufanyike uhamasishaji wa
watu kupima afya hususani wa magonjwa yasiyoambukiza. Tiba ya mapema inapunguza
uwezekano wa kupatwa na madhara zaidi.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Chemba Saimon Odunga ambaye alimwakilisha Mkuu wa
Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amewakaribisha washiriki wa tamasha hilo
mkoani Dodoma ambalo limeshirikisha washiriki kutoka ndani na nje ya mkoa huo
na hata nje ya nchi.
Odunga
amewataka wakazi na wananchi wa mkoa wa Dodoma kutumia fursa ya tamasha hilo
kwa kushiriki michezo mbalimbali hatua ambayo itwasaidia watu na jamii nzima
kuweka afya zao katika hali bora ambayo inawatenga na magonjwa yasiyoambukiza.
Tamasha
hilo ni la wiki moja ambalo limeandaliwa na kuratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto kwa kushirikiana na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Sekretarieti ya Mkoa wa Dodoma, pamoja na Wizara ya Ofisi ya Rais TAMISEMI ambapo
limeshirikisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, pete, kikapu pamoja
mchezo wa kuvuta kamba. Tamasha hilo linaongozwa na kauli mbiu yetu ya mwaka
huu; “Tutembee Pamoja Katika Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa Yasiyoambukiza”
Katibu
Mkuu Wazara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi (wa pili
kushoto) akishiriki mazoezi wakati wa
ufunguzi wa tamasha la michezo la wiki ya kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyo
ambukiza leo jijini Dodoma. Wa pili kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Naibu Katibu Mkuu (Afya) Dkt.
Zainabu Chaula.
Watumishi
wa Umma waliendelea na mazoezi mbalimbali leo uwanja wa Jamhuri Dodoma wakati
wa ufunguzi wa tamasha la michezo la wiki ya kuzuia na kudhibiti magonjwa
yasiyo ambukiza.
Watumishi
wa Umma waliendelea na mazoezi mbalimbali leo uwanja wa Jamhuri Dodoma wakati
wa ufunguzi wa tamasha la michezo la wiki ya kuzuia na kudhibiti magonjwa
yasiyo ambukiza.
(Picha
na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma)
Venance Mwamoto Mbunge wa
Kilolo ni akiendelea na mazoezi kabla ya ufunguzi wa tamasha la michezo la wiki
ya kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyo ambukiza leo jijini Dodoma wakati timu
ya Bunge akijiandaa na mchezo dhidi ya watumishi wa umma leo katika uwanja wa
Jamhuri Dodoma.
Katibu
Mkuu Wazara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi (wa pili
kushoto) akishiriki mazoezi wakati wa
ufunguzi wa tamasha la michezo la wiki ya kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyo
ambukiza leo jijini Dodoma. Wa pili kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Naibu Katibu Mkuu (Afya) Dkt.
Zainabu Chaula.
Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza akito vifaa vya
michezo mbalimbali wakatimwa ufunguzi wa tamasha la michezo la wiki ya kuzuia
na kudhibiti magonjwa yasiyo ambukiza leo jijini Dodoma.
Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza akito vifaa vya
michezo mbalimbali wakatimwa ufunguzi wa tamasha la michezo la wiki ya kuzuia
na kudhibiti magonjwa yasiyo ambukiza leo jijini Dodoma.
Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza akito vifaa vya
michezo mbalimbali wakatimwa ufunguzi wa tamasha la michezo la wiki ya kuzuia
na kudhibiti magonjwa yasiyo ambukiza leo jijini Dodoma.
(Picha na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma)
No comments:
Post a Comment