Habari za Punde

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Anayeshughulikia Muungano na Mazingira Mhe. Goerge Simbachawene Aendelea na Ziara Yake Kisiwani PembaE AWATAKA WATENDAJI KUZINGATIA SHERIA WANAPOSIMAMIA MIRADI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene (wa pili kushoto) akiwa na wabunge wa majimbo ya Pemba katika ziara kutembelea miradi ya Mfuko wa Jimbo wilaya za Wete na Chakechake.

Na.Robert Hokororo. -Pemba.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene amewataka watendaji wa Serikali wanaosimamia miradi mbalimbali ya maendeleo kuzingatia sheria wanapotekeleza shughuli zao.

Mhe.Simbachawene ametoa kauli hiyo wilayani Chakechake, Pemba wakati wa majumuisho ya ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi ya Mfuko wa Jimbo katika wilaya za Wete na Chakechake kisiwani Pemba.

Alisema kuwa Katika kuhakiksha mfuko unatekelezwa vizuri watendaji hao wana wajibu wa kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika hatua zote za utekelezaji wa miradi ili mwishoni waweze kuandika taarifa.

Akizungumza na wabunge wa majimbo yaliyopo katika wilaya hizo pamoja na watendaji hao alibainisha kuwa nafasi ya mbunge na kamati inayosimamia mradi kupitia Mfuko wa Jimbo ni kubwa na wanapaswa kufanya kazi hadi kukamilika kwake.  

“Wajibu wa kamati unaendelea hadi mradi ukamilike kwani baadaye mtatakiwa kuandika ripoti ya nini kimefanyika tangu mwanzo wa mradi hivyo kukataa kushirikiana na mbunge hakuna tija ni kinyume cha utaratibu na sheria na pia mbunge anapaswa kusimamia mradi kuona kama kuna value for money,” alisisitiza.

Awali wakitoa maoni yao kwa waziri baadhi ya wabunge akiwemo Maida Hamed Abdallah wa Viti Maalumu Mkoa wa Kaskazini Pemba waliomba wawe wanashirikishwa katika kamati za miradi ndani ya majimbo pamoja na kuwa wao hawana mufuko wa jimbo.

Walisema kuwa kutokana na wao kutokuwa sehemu ya kamati inakuwa ni jambo gumu kuweza kulitolea ufafanuzi wa namna gani fedha za mfuko zimetumika kwakuwa wanakosa taarifa muhimu.

Miradi aliyotembelea Simbachawene ni mradi wa skuli ya maandalizi Kangagani na mradi wa maji safi na salama Wingwi Mjazana iliyopo Wilaya Wete. Pia alitembelea miradi skuli ya Vikungani na mradi wa umeme wa Pujini iliyopo Wilaya ya Chakechake., 

Waziri Simbachawene katika ziara hiyo pia alitembelea Ofisi ya Makamu wa Rais iliyopo Tunguu, Unguja ambapo alipata nafasi ya kukutana na baadhi ya watumishi na kusalimiana nao.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene akiwa katika skuli ya maandalizi ya Kangagani wakati wilayani Wete, Pemba wa ziara ya kutembelea miradi ya Mfuko wa Jimbo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na wabunge alioambatana nao kwenye ziara ya kukagua miradi ya Mfuko wa Jimbo wilaya za Wete na Chakechake mara baada ya kuwasili Ofisi za Makamu wa Pili wa Rais Pemba.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene akizungumza wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara wilayani Chakechake. Kulia kwake ni Mbunge wa Mtambile, Mhe. Masoud Abdallah Salim.
Wabunge wa majimbo ya Pemba wakiwa katika kikao cha majumjisho ya ziara ya kukagua miradi ya Mfuko wa Jimbo katika wilaya za Wete na Chakechake.
Wataalamu kutoka halmashauri za wilaya na mabaraza ya miji wakiwa katika kikao cha majumjisho ya ziara ya kukagua miradi ya Mfuko wa Jimbo katika wilaya za Wete na Chakechake.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene (katikati)n akiendesha kikao cha majumuisho ya ziara ya kukagua miradi ya Mfuko wa Jimbo wilaya za Wete na Chakechake. Kushoto ni Mbunge wa Mtambile, Mhe. Masoud Abdallah Salim na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais Lupi Mwaikambo.

Kaimu Mkurugenzi wa Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais Lupi Mwaikambo akifafanua jambo katika kikao cha majumjuisho ya ziara ya kukagua miradi ya Mfuko wa Jimbo wilaya za Wete na Chakechake, Pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.