Kaimu Katibu Mkuu
Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo Dkt.Ally Possi (kulia) akipokea
zawadi ya Kamusi Kuu ya Kiswahili
iliyoandaliwa na Baraza la Kiswahili la Taifa kutoka kwa Katibu
Mtendaji Baraza la Kiswahili la
Taifa Dkt.Selemani Sewangi leo Jijini
Dar es Salaam alipotembela ofisi hiyo kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa
majukumu.
Na. Anitha Jonas –
WHUSM,Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Dkt.Ally Possi
amewataka wafanyakazi wa Baraza
la Kiswahili Taifa kuwa wabunifu wa
miradi itakayoliletea taifa matokeo chanya katika kutangaza lugha ya Kiswahili
kwenye nyanja za Kimataifa .
Dkt.Possi ametoa
kauli hiyo leo Jijini Dar es Salaam
alipotembelea ofisi za baraza hilo kwa lengo kupata taarifa za utekelezaji wa mpango
mkakati wake pamoja na kufahamu malengo ya taasisi hiyo katika kipindi cha kwanza
kwa mwaka wa fedha 2019/2020.
“Nawapongeza kwa
mradi huu mzuri wa Kongoo sababu kazi mnayofanya yakuingiza maneno tabribani billion
moja ya Kiswahili katika mtandao itasaidia
sana kukuza na kusambaza lugha
hii kwani sasa dunia imejikita zaidi katika tehama na shughuli nyingi
zinafanyika kwa njia ya mtandao hivyo
uhifadhi wa maneno hayo ya Kiswahili katika mfumo huu ni hatua nzuri,”Dkt.Possi.
Akiendelea kuzungumza
katika ziara hiyo Kaimu Katibu Mkuu huyo aliendelea kusisitiza kuwa BAKITA ni
taasisi muhimu kwa taifa na wizara ipo tayari kwa kuwawezesha kufanikiwa
kutekeleza majukumu yake ya kuweza kufanikisha lugha hiyo inasonga mbele sababu kukua kwa lugha
hiyo ni ufahari kwa Tanzania na haswa kama waasisi wa kutumia hugha hiyo.
Pamoja na hayo nae
Katibu Mtendaji wa BAKITA Dkt.Selemani Sewangi
alitoa maombi Kaimu Katibu Mkuu huyo ya kuomba wizara iwasaidie katika
kutangaza katika wizara mbalimbali kuwa wanauza Kamusi Kuu ya lugha ya
Kiswahili iliyoandaliwa na baraza hilo yenye maneno mengi kwani
uandaaji wa kamusi za Kiswahili ni moja ya majukumu yao.
“Tungependa baraza lianze kutoa mafunzo ya ukalimani kwa wahitimu wa
chuo kikuu na wadau mbalimbali sababu tumeona kuna ombwe kubwa la wataalamu wa lugha wanaoweza kufanya kazi ya ukalimani hivyo
tungeomba kupatiwa fedha ili kuweza kufanikisha kununua vifaa vya kutoa mafunzo
hayo,”alisema Dkt.Sewangi.
Halikadhalika
Dkt.Sewangi aliwashukuru uongozi wa
wizara kwa kuwapa ahadi ya kushughulikia suala ya baraza hilo kupata kiwanja
cha kujenga ofisi ndani ya Jiji la
Dodoma ambapo ndiyo Makao Makuu ya Ofisi za Serikali .
Mbali na hayo nae
mmoja wa wafakakazi wa baraza hilo ambaye ni Mfasiri Mkuu Bibi. Vidah Mutasa alitoa neno la shukrani baada kumalizika kwa
kikao hicho cha kiongozi huyo wa wizara na wafanyakazi wa baraza kwa kuahidi
kuchapa kazi na kuhakikisha wao kama mabalozi wa lugha hiyo wanahakikisha
inasonga mbele.
No comments:
Post a Comment