Habari za Punde

NEMC, MGODI WA NORTH MARA WASAINI MAKUBALIANO YA UZINGATIAJI SHERIAYA MAZINGIRA

Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi Emma Lyimo (kulia) akikabidhiana nyaraka na Meneja Mkuu wa Mgodi wa North Mara, Luiz Correia mara baada ya kushuhudia utiaji saini wa mkataba baina ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na mgodi huo kwa ajili ya utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu uzingatiaji wa Sheria za nchi ikiwemo Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake katika utekelezaji wa shughuli za migodi. Hafla hiyo imefanyika leo katika Ofisi za Makamu wa Rais jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Samuel Gwamaka (kushoto) akikabidhiana nyaraka na Meneja Mkuu wa Mgodi wa North Mara, Luiz Correia baada ya utiaji wa saini mkataba baina ya NEMC na mgodi huo kwa ajili ya utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu uzingatiaji wa Sheria za nchi ikiwemo Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake katika utekelezaji wa shughuli za migodi.
Wajumbe kutoka Mgodi wa North Mara na Baraza la Taifa la  Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakipitia nyaraka kabla ya kutiliana saini kwa mkataba baina yao kwa ajili ya utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu uzingatiaji wa Sheria za nchi ikiwemo Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake katika utekelezaji wa shughuli za migodi. 
Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Samuel Gwamaka akisaini mkataba kwa ajili ya utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu uzingatiaji wa Sheria za nchi ikiwemo Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake katika utekelezaji wa shughuli za migodi. 

Mkuu wa Kitengo cha Mazingira kutoka Mgodi wa North Mara, Bw. Tunzo Msuya akisaini mkataba baina yao kwa ajili ya utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu uzingatiaji wa Sheria za nchi ikiwemo Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake katika utekelezaji wa shughuli za migodi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.