Na.Shamimu
Nyaki-WHUSM, Dodoma
Shirika
la Utangazaji Tanzania (TBC) ni chombo cha Habari cha Umma chenye wajibu wa
kuhabarisha kuelimisha pamoja na kueleza mikakati ya Serikali katika kuleta
maendeleo kwa wananchi.
Katika
kuhakikisha yote hayo yanafanyika Serikali inafanya juhudi kubwa za kuimarisha
usikivu wa Shirika hilo katika mikoa yote ya Tanzania ili wananchi wapate
taarifa sahihi zilizokusudiwa tena kwa
wakati.
Moja
ya mikakati ambayo Serikali imeweka katika kuimarisha usikivu wa Shirika hilo
ni kubadilisha mitambo ya zamani na kuweka mipya na kuhamisha mitambo kutoka
sehemu ambayo mawimbi ya FM hayafiki na kuipeleka maeneo ya vilima vilivyopo juu
zaidi ambapo wataalamu wameona kuwa ndio maeneo sahihi yatakayosaidia kupeleka
mawimbi ya redio na televisheni kuwafikia wananchi nchi nzima.
Shirika
hili chini ya uongozi wake Mkurugenzi Mkuu Dkt. Ayoub Ryoba linaendelea kuweka
mipango na mikakati ya kuhakiksha wananchi wanapata habari ambapo matarajio ni
kukakikisha usikivu wa redio unzifikia wilaya 117 nchi nzima.
Serikali
imefanya mageuzi makubwa katika kuhakikisha usikivu unaimarika ambapo umeongezeka kutoka Wilaya 87 mwaka 2017 sawa
na asilima 54 hadi wilaya 102 mwaka 2019 ambapo pia imejenga vituo vitano
ambavyo tayari ujenzi wake umekamilika na vimeanza kutumika. Wilaya za mpakani
ndizo zimenufaika na ujenzi huo ikiwemo Rombo, Kibondo, Tarime, Kankonko,
Longido eneo la Namanga, Nyasa hadi Mbambabay.
Yapo
ameneo ambayo usikivu ni hafifu hali ambayo imeilazimu Serikali kuweka mitambo
ya redio katika ameneo yenye changamoto hiyo ambayo katika mikao mitano ya
Lindi, Katavi, Njombe, Simiyu, Songwe ambapo nguvu hiyo pia inaelekezwa katika
mikoa ya Unguja na Pemba..
Hivi
karibuni Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza
amesema kuwa TBC inaendelea na mpango wa kupanua usikivu maeneo yote ya nchi
ili wananchi wengi wapate manufaa ya shirika lao ambapo amesema lengo la
Serikali ni kuiwezesha TBC Redio kufikia usikivu nchi nzima kama ambavyo TBC
Televisheni inaonekana kupitia visimbuzi na satellite vyote zilizosajiliwa
nchini.
Ni
dhahiri ziara ya Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison
Mwakyembe aliyoifanya hivi karibuni katika mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha,
Manyara na Singida ilikuwa ni muendelezo wa ziara za kikazi ambayo ilikuwa na lengo
la kuona na kujiridhisha kuhusu usikivu wa TBC katika maeneo hayo na hatua
zilizochukuliwa na shirika hilo katika kutatua changamoto zinazowakabili ili kuhakikisha
matangazo ya redio yanawafikia wananchi wote inavyotakaiwa kwa wakati ikiwa ni
haki yao ya msingi ya Kikatiba ya kupata taarifa za Serikali.
Akiwa katika Mkoa wa Tanga Dkt.
Mwakyembe alisema kuwa Serikali inaendelea kuboresha usikivu wa matangazo ya
Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kwa kuimarisha mitambo ya kurushia
matangazo katika kituo cha Mnyusi kilichopo Hale wilaya ya Korogwe na Kwemashai
wilaya ya Lushoto mkoani Tanga.
Dkt. Harrison Mwakyembe alisema
kuwa usikivu wa TBC Taifa mwaka 2015 ulikuwa ni asilimia 54 ambapo kwa sasa
baada ya Serikali kuboresha vituo hivyo usikivu umefikia kiwango cha asilimia
73 na inatarajiwa ifikapo mwishoni mwa mwaka 2020 utafikia zaidi ya asilimia
90.
Katika Mkoa wa Kilimanjaro
Waziri Mwakyembe alitembelea kituo cha TBC Taifa Mabungo kilichopo wilayani
Moshi kinachorusha matangazo katika masafa ya FM 87. 9 Mhz na TBC FM katika
masafa ya 90.0 Mhz pamoja na kituo cha Tarakea kilichopo katika Wilaya ya Rombo
ambacho matangazo ya TBC Taifa yanapataikana kupitia masafa ya 87.9Mhz na TBC
FM inarusha kupitia 90.0 Mhz.
Akiwa mkoani Arusha
Dkt.Mwakyembe alitembelea eneo la Themi ambalo ndio mitambo ya TBC imewekwa
ambayo inarusha matangazo yake kupitia masafa ya 89.9 Mhz kwa FM na 87.7 Mhz
pamoja na kituo cha cha Namanga kilichopo katika Wilaya la Longido.
Hata hivyo usikivu umeendelea
kuimarishwa katika mikoa ya Singida pamoja na Manyara ambayo pia Waziri mwenye
dhamana ya habari alifanya ziara ya kikazi katika mikoa hiyo kukagua hali ya
usikivu na kupokea taarifa kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dkt. Ayoub Ryioba ambaye
alitoa taarifa kuwa mkoa wa Singida ulikua na changamoto ya usikivu baada ya
mtambo kuharibika ambapo tayari Serikali imechukua hatua ya kutafuta mitambo
mingine.
Dkt. Ryoba amesema kuwa mitambo
miwili ya Khts 2 sawa na Wats 2000 imeshawasili nchini tayari kwa kufungwa
katika eneo la Mikumbi Mkoani hapo ili kuongeza usikivu katika maeneo mengi ya
mkoa huo ambao matarajio ni kuimarisha usikivu kwa zaidi ya asilimia 70
mwishoni mwa mwaka huu.
“Hizi jitihada kubwa kwa
Serikali za kuhakikisha kuwa inatekeleza
Ibara ya 18 d ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoeleza
kuwa kila mwananchi ana haki ya kupata taarifa sahihi, hivyo ni jukumu la
Serikali kuweka mazingira bora kwa vyombo vya habari kutoa habari bila
changamoto zozote na kuzifikisha kwa
walengwa kwa usahihi na kwa wakati” alisisitiza Dkt. Mwakyembe.
Aidha, Dkt. Mwakyembe alipata
pia fursa ya kutembelea mkoa wa Manyara ambapo tayari Serikali imeanza
kuhamisha mitambo ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kutoka katika jengo
la Mkoa wa Manyara kupeleka katika eneo la Gitsmii ambalo lina mwinuko
utakaosaidia kuimarisha usikivu katika mkoa huo ambao nao una kabiliwa na
changamoto ya kutosikika vizuri kwa matangazo ya TBC katika maeneo mengi.
Waziri Mkwayembe alisema kuwa
Serikali inafahamu changamoto ya usikivu wa TBC Manyara ndio maana wataalam
wamekuja na suluhisho la changamoto hiyo ya kuhamisha mtambo kupeleka eneo
ambalo wameona litarahisisha upatikananji wa wa matangazo vizuri.
Katika ziara yake katika mikoa
hiyo, Waziri amejionea changamoto ya miundombinu mibovu ya kufika eneo la
mitambo ambapo alitoa maagizo kwa mikoa hiyo kushirikiana na TANROADS, TANESCO
pamoja na Idara ya Maji kutatua changamoto hizo za barabara pamoja na umeme ili
kuhakikisha wanaweka miundombinu rafiki kwa ajili ya ulinzi wa mali ya umma kwa
manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla.
Dkt. Mwakyembe alieleza kuwa
barabara za kuelekea kituo cha Gitsmii Manyara, Mnyusi Hale pamoja na kwemashai
Lushoto zinapaswa kujengwa kwa lami au zenge kwakuwa sehemu hizo zina miinuko
mikali pamoja kona nyingi, ambapo vituo vya Namanga Wilayani Longido, Mbungo
Moshi na Themi Arusha vinahitaji barabara ya lami pia.
Hata hivyo Wakuu wa Mikoa hiyo wameahidi
kutekeleza maagizo hayo ambayo ni kipaumbele kwa wananchi ili waweze kupata
matangazo ya redio yao kwa kuwa ina lengo la kuhabarisha, kuelimisha, kuonya
pamoja na kuburudisha na wameunga mkono jitihada za Serikali za kuimarisha
usikivu katika maeneo yao.
Kwa upande wao Mkuu wa wilaya
ya Longido Frank Mwaisumbe na Agnes Hokororo wilaya ya Rombo wamesema kuwa kwa
sasa TBC imekuwa chanzo kikuu kwa wananchi wa wilaya zao kupata taarifa za maendeleo ya nchi zao tofauti na hali
ilivyokuwa miaka ya nyuma ambapo wananchi walikuwa wakipata taarifa kutoka nchi
za jirani
Wananchi katika mikoa ambayo
Waziri Dkt. Mwakyembe alitembelea wamesema kuboreshwa miundombinu kufika maeneo
ambayo TBC imesimika mitambo yake ya kurusha matangazo ikiwemo barabara, umeme
na maji itasidia pia kuboresha maisha yao kiuchumi na kijamii na itasaidia kuwa
kiunganishi kikubwa katika kuleta maendeleo ya kaya zao pamoja na Taifa.
No comments:
Post a Comment