Afisa Msimamizi wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi. Julieth Kidemi akiwaelimisha wakazi wa Mbuyuni kata ya Kimbiji wilayani Kigamboni kuhusu madhara mbalimbali yatokanayo na biashara za magendo wakati wa kampeni maalum ya kuelimisha wananchi kuhusu athari za magendo katika ukanda wa Bahari ya Hindi. Kampeni hii imeanza kufanyika tarehe 3 na itamalizika tarehe 11 Februari, 2020 katika maeneo mbalimbali ya Dar es Saalam, Pwani, Tanga, Mtwara na Lindi.
Afisa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Ernest Mngube akiwaelimisha wakazi wa kata ya Kimbiji wilayani Kigamboni kuhusu madhara mbalimbali yatokanayo na biashara za magendo wakati wa kampeni maalum ya kuelimisha wananchi kuhusu athari za magendo katika ukanda wa Bahari ya Hindi. Kampeni hii imeanza kufanyika tarehe 3 na itamalizika tarehe 11 Februari, 2020 katika maeneo mbalimbali ya Dar es Saalam, Pwani, Tanga, Mtwara na Lindi.
Afisa Msimamizi wa Kodi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Rose Mahendeka akiwaelimisha wakazi wa kata ya Kimbiji wilayani Kigamboni kuhusu madhara mbalimbali yatokanayo na biashara za magendo wakati wa kampeni maalum ya kuelimisha wananchi kuhusu athari za magendo katika ukanda wa Bahari ya Hindi. Kampeni hii imeanza kufanyika tarehe 3 na itamalizika tarehe 11 Februari, 2020 katika maeneo mbalimbali ya Dar es Saalam, Pwani, Tanga, Mtwara na Lindi. na Lindi.
Mmoja wa wakazi wa Mbuyuni kata ya Kimbiji wilayani Kigamboni akitoa maoni yake wakati wa kampeni maalum ya kuelimisha wananchi kuhusu athari za magendo katika ukanda wa Bahari ya Hindi iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kampeni hii imeanza kufanyika tarehe 3 na itamalizika tarehe 11 Februari, 2020 katika maeneo mbalimbali ya Dar es Saalam, Pwani, Tanga, Mtwara na Lindi.
Wakazi wa kata ya Kimbiji wilayani Kigamboni wakimsikiliza kwa makini Afisa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Ernest Mngube (hayupo pichani) wakati wa kampeni maalum ya kuelimisha wananchi kuhusu athari za magendo katika ukanda wa Bahari ya Hindi iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kampeni hii imeanza kufanyika tarehe 3 na itamalizika tarehe 11 Februari, 2020 katika maeneo mbalimbali ya Dar es Saalam, Pwani, Tanga, Mtwara na Lindi.
Na
Veronica Kazimoto. Kigamboni
Wakazi na wafanyabiashara
waishio pembezoni mwa fukwe za Bahari ya Hindi katika kata za Somangila,
Kimbiji na Pemba Mnazi zilizopo Wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam
wameelimishwa kuhusu athari za magendo yanayopitishwa kinyume na sheria katika
maeneo hayo.
Elimu hiyo imetolewa wakati
wa kampeni maalum ya kuelimisha wananchi kuhusu athari za magendo katika ukanda
wa Bahari ya Hindi iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambayo
inafanyika maeneo mbalimbali katika mikoa ya Dar es Saalam, Pwani, Tanga,
Mtwara na Lindi.
Akizungumza na wakazi hao
katika maeneo ya Buyuni na Kimbiji wilayani Kigamboni, Afisa Kodi Mkuu Rose
Mahendeka kutoka mamlaka hiyo, amewaambia wakazi hao kuhakikisha wanatoa
taarifa pindi wanapoona bidhaa za magendo ikiwa ni pamoja na kuepuka kutumia
bidhaa hizo kwani zinaweza kuwa na madhara kwa afya zao.
“Ndugu zangu athari za
magendo siyo tu kukwepa kodi ya serikali, lakini pia bidhaa hizo zinazopita
katika njia zisizo rasmi, zinakuwa hazijathibitishwa na Shirika la Viwango
Tanzania (TBS) na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) na hivyo zinaweza kuwaletea
madhara kiafya,” alisema Mahendeka.
Naye, Afisa Forodha kutoka
TRA Ernest Mngube, amewaasa wafanyabiashara wanaojishughulisha na biashara za
magendo kuacha tabia hiyo mara moja kwani wakibainika licha ya kuchukuliwa
hatua za kisheria, watataifishiwa bidhaa zao ikiwa ni pamoja na vifaa
vilivyotumika kubeba au kuhifadhi bidhaa hizo.
“Ni muhimu wafanyabiashara
mtambue kwamba kupitisha bidhaa katika njia zisizo rasmi ni kinyume na sheria
na mkibainika siyo tu mtachuliwa hatua kwa mujibu wa sheria bali bidhaa zenu
zitataifishwa pamoja na vifaa kama gari, pikipiki, mashua zinazotumika bidhaa
hizo na hata majengo yatakayokutwa yamehifadhi magendo hayo,” aliwaasa Mngube.
Mgumbe amezitaja namba
ambazo wananchi wanaweza kutoa taarifa kila wanapoona biashara za magengo
katika maeneo yao ambazo ni 0746 23 24 91, 0800 75 00 75, 0800 78 00 78 au kutuma
ujumbe wa whatsapp kwenda namba 0744 23 33 33 au kutuma barua pepe kwenda huduma@tra.go.tz.
Kampeni maalum ya kuelimisha
wananchi kuhusu athari za magendo katika ukanda wa Bahari ya Hindi imeanza
kufanyika tarehe 3 na itamalizika tarehe 11 Februari, 2020 katika maeneo
mbalimbali ya Dar es Saalam, Pwani, Tanga, Mtwara na Lindi ikiwa na lengo la
kuwaelimisha wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla madhara mbalimbali
yatokanayo magendo hayo.
No comments:
Post a Comment