Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz kulia akikabidhi
msaada wa vitu mbalimbali kwa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha
Ngamiani Jijini Tanga Anjelina Mashaka kushoto kwa ajili ya wakina mama
wajawazito wanaojifungua kwenye kituo hicho katikati anayeshuhudia
ni Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro
Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz kulia akikabidhi
msaada wa vitu mbalimbali kwa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha
Ngamiani Jijini Tanga Anjelina Mashaka kushoto kwa ajili ya wakina mama
wajawazito wanaojifungua kwenye kituo hicho katikati anayeshuhudia
ni Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro
Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz kulia akikabidhi
msaada wa vitu mzazi aliyemkuta kwenye wodi ya wakina mama wajazito kwenye Kituo cha Afya cha
Ngamiani Jijini Tanga kushoto ni kwa ajili ya wakina mama
wajawazito wanaojifungua kwenye kituo hicho leo katikati anayeshuhudia
ni Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro
Afisa
Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz akizungumza mara baada ya
kutoa msaada huo kulia ni Mkurugenzi wa Mashindano wa Klabu ya Yanga
Thabithy Kandoro
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha
Ngamiani Jijini Tanga Anjelina Mashaka akizungumza huku akiishukuru Klabu ya Yanga kwa msaada huo
Mkurugenzi
wa Mashindano wa Klabu ya Yanga Thabithy Kandoro akizungumza mara baada
ya makabidhiano hayo kushoto ni Afisa Mhamasishaji wa klabu hiyo
Antonio Nugaz
Afisa
Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaza kushoto akiwaongoza
wanachama na wapenzi wa klabu hiyo kuingia kwenye kituo cha Afya
Ngamiani Jijini Tanga kwa ajili ya kutoa msaada .
KLABU
ya Yanga imetoa msaada wa vitu mbalimbali kwenye wodi ya wakina mama
wajawazito kwenye kituo cha Afya Ngamiani Jijini Tanga ikiwa ni mkakati
wao kusaidia makundi mbalimbali kila wanapo kwenda kucheza mechi zao za
ligi kuu ikiwa ni mpango wao wa kurudisha kwa jamii.
Msaada huo
umekabidhiwa leo na Afisa Mhamasishaji wa Klabu ya Yanga Antonio Nugaz
kwa Mganga Mfawidhi wa kituo hicho Anjelina Mashaka katika halfa
iliyohudhuriwa mashabiki na wanachama wa timu hiyo mkoani Tanga.
Akizungumza
wakati akikabidhi msaada huo Nugaz alisema wana mshukuru Mwenyezi Mungu
amewawezesha kuwqa sehemu ambazo wazazi wao ambao walizaliwa kwenye
vituo mbalimbali vya afy na wao wamefika kwenye kituo hicho kwa kile
walichobarikiwa wakiotoe wodi ya wakina mama.
Alisema msaada
ambao wameutoa pamoja na vitu vyengine lakini neti za kujikinga na mbu
ambazo wamezikabidhi zitakuwa msaada mkubwa kwao ili kuepukana na kuumwa
ugonjwa wa malaria.
“Wazazi ambao wamebahatika kupata watoto
wanapaswa kujikinga na mbu ambao wanaeneza malaria hivyo katika
kurudisha kwa jamii timu ya wananchi tumeona tuwasaidia neti na vitu
vyengine ikiwemo sabuni na vifaa kwa ajili wa watoto wadogo”Alisema
Mhamasishaji huyo.
Aidha alisema kwamba amefurahishwa na namna
wanachama wa Yanga na mashabiki waliovyoonyesha mshikamano wa pamoja
kwenye jambo hilo hivyo kwa niaba ya kamati ya utendaji chini ya
Mwenyekiti wao Dkt Mshindo Msola na timu nzima.wanakwenda kuchukua
pointi tatu ingawa mechi itakuwa ni ngumu.
Awali akizungumza
katika halfa hiyo Mganga Mfawidhi wa kituo hicho Anjelina Mashaka
aliishukuru klabu hiyo kwa kuona umuhimu wa kuwasaidia msaada huo ambao
umefika wakati muafaka.
“Nashukuru kupokea neema ambazo
mmezileta Yanga kwa niana ya Jiji la Tanga natoa shukrani zangu za dhati
kwa ajili ya zawadi na wagonjwa wetu ambao wanajiandaa kupata
watoto”Alisema Mganga huyo
Alisema kwamba pia wanathamini
mchango wao wa kutoa sadaka kwap ambao utawasaidia kutokana na hapo
awali kuwa na uhitaji wa neti ambazo zitasaidia kwenye kituo hicho.
Hata
hivyo Mkurugenzi wa Mashindano wa timu ya Yanga Thabithy Kandoro
alisema kwamba timu halisi ya Yanga lazima iende kwa vitendo ni jambo la
msingi wao.
Alisema wao kama timu ya wananchi wana sababu ya
kuijenga timu yao na kuwa wazalendo na kuhakikisha wananchi wanafaidi na
kupata afadhali watu wengine wajitokeze kuwasaidia watu wenye mahitaji
mbalimbali.
No comments:
Post a Comment