Na.Himid Choko. Zanzibar.
Waziri wa Biashara na Viwanda Balozi
Amina Salum Ali amesema , Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea
kuweka mipango madhubuti, ili kukifanya
kilimo cha mwani kuwa na manufaa zaidi kwa wakulima na taifa kwa
jumla.
Amesema miongoni mwa mikakati
inayochukuliwa nI pamoja na kuwapatia wakulima wa zao hilo wataalamu wa kisasa
ambao wanaendelea kuwapatia mafunzo na utaalamu wakulima wa mwani hapa nchini.
Amesema kutokana na taaluma nzuri
wanayopatiwa wakulima hao , hivi sasa wamekuwa wakivuna zaidi ya kilo tatu kwa mbegu moja ukilinganisha na hapo awali.
Balozi Amina amesema hayo leo
wakati akitowa ufafanuzi wa hoja mbai
mbali za wajumbe wa baraza la Wawakilishi kuhusiana na utekelezaji wa Maagizo
ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi ya Mwaka
2019/2020 kwa Wizara ya Biashara na Viwanda.
Mheshhimiwa
Balozi Amina amelieleza Baraza la Wawakilishi kua, faida nyengine ya
elimu ya ukulima wa mwani ni
kuongeza ubora wa zao hilo na hivyo
kusababisha kupanda kwa bei ya mwani kutoka shilingi 400 hadi shilingi 1,800
kwa kilo hivi sasa.
Amesema katika hatua nyenginige
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inakusudia kujenga kiwanda cha Usarifu wa
mwani huko Chamanangwe Pemba ndani ya Awamu hii ili kuongeza soko na thamani ya
zao hilo.
Imetolewa na Divisheni ya Itifaki na Uhusiano,
Baraza la Wawakilishi, Zanzibar.
Jumatatu, Aprili 14, 2020
No comments:
Post a Comment