TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA Kitalu Na. 339, Mtaa wa Nyerere - Kilimani
S.L.P 4019, DODOMASimu: +255 734 047 775; 734 119 978
Barua Pepe: info@chragg.go.tz
|
Aprili 23, 2020
TAARIFA
KWA UMMA
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na Tahadhari dhidi
ya Kusambaa kwa Virusi vya Corona
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) kwa
kuzingatia tamko la Serikali kuhusu tahadhari ya kusambaa kwa ugonjwa wa COVID-19
unaosababishwa na virusi vya Corona, inatoa mwongozo ufuatao, unaopaswa
kuzingatiwa na wananchi wote wanaofika katika ofisi za Tume kwa ajili ya kupata
huduma mbalimbali:-
1. Wananchi wote wanaotarajia kufika ofisi za Tume kwa ajili
ya kuwasilisha na kufuatilia malalamiko yao, ama kwa shida nyingine za ki-ofisi
na binafsi wawe wamevaa barakoa.
2. Wananchi walio na malalamiko yanayohusisha kikundi cha
watu, wateuwe wawakilishi wasiozidi wawili (2) watakaofika Tume kuwawakilisha
badala ya kufika kwa kikundi.
3. Aidha, katika kipindi hiki Wananchi wanahimizwa kutumia
zaidi utaratibu wa kuwasilisha malalamiko bila kufika ofisi za Tume kwa kutumia
njia ya barua, ujumbe mfupi wa simu ya kiganjani (SMS), simu na barua pepe
(e-mail) kwa kutumia anuani na namba za simu zilizopo hapa chini.
Mawasiliano yote yaelekezwe kwa Mwenyekiti, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. Kwa
kutegemeana na mahali ulipo, tuma barua yako kwa kutumia moja ya anuani
zifuatazo:
S.L.P. 1049, DODOMA; Simu: 0734 047 775/0734 119 978; Barua pepe: info@chragg.go.tz
au
S.L.P. 285, ZANZIBAR; Simu: (024) 2230494/236124 au
S.L.P. 2643, 11101 DAR ES SALAAM; Simu: (022) 2135747/8; Barua pepe: info@chragg.go.tz
au
S.L.P. 10430, MWANZA; Simu: (028) 2541770; Faksi (028) 2541770 au
S.L.P. 1050, LINDI; Simu: (023) 2202734/2202744 au
S.L.P. 231, WETE – PEMBA; Simu: (024) 2454196.
Kuwasilisha lalamiko kwa njia ya
ujumbe mfupi
Tuma ujumbe wa simu ya kiganjani (SMS) kwenda Na. 0737 446 787, ukianzia na neno ‘REPORT’. Mfano: REPORT Shule ya Msingi Kinondoni, DSM
tunachapwa viboko zaidi ya 10.
Kufuatilia lalamiko
lililokwisha wasilishwa
Tuma ujumbe wako ukianza na neno ‘STATUS’ kwenda Na. 0737
446 787. Mfano: STATUS
13024 (13024 ni mfano wa namba ya lalamiko atakayokuwa amepewa Mlalamikaji).
Kwa maelezo zaidi piga simu Na. 0734 047 775/0734 119 978 au tuma barua pepe
kwenda: info@chragg.go.tz
MUHIMU: Mlalamikaji aandike jina, anwani yake, namba ya simu na anuani
ya barua pepe (kama anazo) ili Tume iweze kuendeleza mawasiliano.
Ni matumaini ya Tume kuwa wananchi watazingatia mwongozo
huu ili kuendelea kufurahia huduma kutoka Tume katika kipindi hiki cha
mapambano dhidi ya gonjwa hatari linalosababishwa na virusi vya Corona.
Imetolewa na:
Mathew Pauwa Mhina Mwaimu (Jaji Mstaafu)
Mwenyekiti
TUME YA
HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
23 Aprili,
2020
No comments:
Post a Comment