Habari za Punde

Naibu Waziri Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said Azindua Kitabu Kuhamasisha Wazee Kuwasomesha Watoto Wao Nyumbani. Hasa Katika Wakati Huu wa Janga la Corona.

Kitabu cha Kuhamasisha Wazzazi kuwa somesha Watoto Wao wakiwa Nyumbani kilichozinduliwa na Naibu Waziri Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar. Mhe.Simai Mohammed Said, hafla ya uzinduzi huo umefanyika katika Ofisi ya Wizara ya Elimu Mazizini Jijini Zanzibar.  

Naibu Waziri Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Simai Mohammed Said akizindua Kitabu chenye ujumbe wa kuhamasisha Wazazi kuwasomesha Watoto wao wanapokuwa majumbani. Uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Elimu Maziziuni Jijini Zanzibar.


Naibu Waziri Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar.Mhe.Simai Mohammded Said akizungumza wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi wa Kitabu cha Kuhamasisha Wazazi kuwasomesha Watoto wao wanapokuwa nyumbani baada ya masomo yao Skuli.



Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe, Simai Mohammed Said amewaomba Wazazi na Walezi kushiriki kikamilifu katika kuwasaidia watoto kuwasomesha wakiwa nyumbani kwao hasa katika wakati huu wa mripuko wa maradhi ya Korona.

Akizungumza wakati alipozindua picha maalum inayohamasisha Wazazi kuwasomesha watoto, huko katika jengo la Wizara hiyo Mazizini Mjini Unguja, Mhe Simai amesema pamoja na kuwa  wazazi wanatoka kwenda katika shughuli zao za kila siku, lakini bado wana jukumu la kuwasimamia watoto wao.

Amesema Wizara ya Elimu Zanzibar itaendelea kuunga mkono Juhudi za Serikali kuhakikisha watoto wanakuwa katika usalama, pia kuhakikisha wanaendelea kupata  Elimu yao wakiwa nyumbani kwao kutokana na kufungwa Skuli na madrasa katika kipindi hiki cha maradhi ya korona,  pamoja na kuendelea kutoa taarifa na maelekezo mbalimbali ya kielimu.

Hivyo amewaomba wazazi kuendelea kuwasimamia watoto wao kwa kuwadhibiti kutoka ovyo katika nyumba zao na kufuata masharti ya wataalamu wa Afya ili kuweza kujikinga na maambukizi ya maradhi hayo.

Nae Naibu Katibu Mkuu Utawala na uendeshaji Wizara ya Elimu, mwalim Abdullah Mzee Abdullah amesema katika kipindi hiki cha kufungwa Skuli kulikosababishwa na kuwepo maradhi ya Korona, Wizara hiyo imeandaa Kamati ya wataalamu kutoka Sekta mbalimbali ili kuandaa mikakati ya kuwawezesha watoto  kusoma wakiwa nyumbani ili kupunguza athari za kufungwa Skuli.

Amesema Kamati hiyo imeweza kuandaa vipindi mbalimbali katika Radio na Runinga, hivyo ni jukumu la wazazi kuvifuatilia kwa karibu vipindi hivyo na kuwa karibu na watoto wao kwa kuwasaidia ili malengo yaweze kufikiwa.

Aidha amewaomba wahisani kuendelea kutoa misaada katika Wizara ya Elimu kutokana na kuwepo kwa baadhi ya jamii kushindwa kumiliki Redio kwa ajili ya kuwapa watoto wao kuweza kufuatilia na kusikiliza masomo hayo.

Pia amesema WEMA inashirikiana na Taasisi ya Elimu Tanzania Bara ambapo  tayari wameandaa masomo ya Sayansi na Hesabu kwa Wanafunzi wa Kidatu cha Tano na Cha sita ambapo tayari wameshakabidhiwa na waakati wowote yataanza kurushwa katika vutuo hivyo vya Radio na Runinga.

Nae Mtendaji Mkuu wa Shirika la Kimataifa kinaloshughulikia masuala ya Elimu Zanzibar UNICEF, bibi Maha Damaj amesema katika kipindi hiki cha kuwepo Maradhi ya Korona hapa Zanzibar ni vizuri WEMA imetoa vipindi hivyo katika vyombo vya Habari ili  watoto wasikae na kutosahau masomo yao.

Hivyo ameishukuru WEMA na kuipongeza kwa hatua nzuri waliyoichukua katika kuwasaidia watoto kupata Elimu kama inavyostahiki.

Kwa upande wake mchoraji wa picha hiyo  Sei Soud Ali ameishukuru Wizara ya Elimu kwa kumuamini kuchora picha hiyo ikiwa ni  mzazi katika kuwahamasisha wazazi wenziwe kuwasimamia watoto wao.

Aidha ameahidi kuendelea kuitumikia nchi yake kwa kuchora picha mbali mbali zenye kutoa Elimu kwa jamii kwa kutimiza
 uzalendo kwa nchi yake.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.