Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi Mhe.Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi, akizungumza na Wananchi na Wanachama wa CCM katika viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Jijini Zanzibar, wakati wa hafla ya mkutano wa mapokezi uliofanyika leo baada ya kuwasili Zanzibar akitokea Dodoma.
Mgombea wa Kiti cha Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi alisema azma ya kugombea wadhifa huo ni
kuwatumikia Wazanzibar pamoja na Watanzania wote kwa uwezo wake wote,
akibainisha dhamira ya kuwaletea maendeleo na ustawi katika maisha yao.
Alisema miongoni mwa vipaumbele vyake
ni pamoja na kuendeleza amani iliopo ili Zanzibar iweze kupiga hatua zaidi za
maendeleo, huku akiahidi kazi hiyo kufanyika kwa ushirikiano kati ya wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama.
Alisema analenga kuimarisha umoja
na mshikamano wa Kitaifa miongoni mwa
Wazanzibari wote ili kuondokana na hatari ya kuibuka kwa ubaguzi wa kimajimbo.
Aidha, alieleza kuwa ataendeleza kasi
ya maendeleo iliyoanzishwa na mtangulizi wake na kukamilisha miradi yote ya
maendeleo kwa maslahi ya Wazanzibari.
Katika utekelezaji wa majukumu yake,
Dk. Mwinyi alisema hatakuwa na muhali, huruma wala na atasimamia vita dhidi ya
rushwa, ubadhirifu wa mali ya umma, uzembe pamoja na watendaji wote wasiowajibika
ipasavyo.
Aliwataka viongozi wa chama hicho
kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa kujiweka tayari kwa kazi ili kuweza kukipatia
ushindi chama hicho, kupitia kampeni zitakazoendeshwa kisayansi ili hatimae kushika Dola.
Katika hatua nyengine, Dk. Mwinyi
aliahidi kutetea maslahi ya Zanzibar kupitia Jumuiya zote za Kikanda na zile za
kimataifa.
Mapema, Naibu Katibu Mkuu wa CCM
Zanzibar Juma Abdalla Sadalla alisema hatua ya kwanza ya uteuzi wa mgombea wa chama
hicho imekamilika, kupitia vikao halali vilivyoendeshwa kwa uwazi na bila
makundi.
Alimsifia mgombea huyo kuwa ni
mwanachama mchapakazi, mweledi, mwenye uelewa wa mambo na uwezo mkubwa katika kutoa maamuzi kwa hekima na
busara.
Mapema kiongozi huyo alipata mapokezi
makubw akutoka kw awnanachi na wanachama wa CCM, waliojikusanya kutoka uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume hadi Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui,
akiwemo msanii maarufu wa kizazi kipya kutoka Tanznaia Bara Ali Kiba.
No comments:
Post a Comment