Waziri
wa Viwanda na Biashara, Mhe.Innocent Bashungwa akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya
Mamlaka ya Biashara Tanzania (Tantrade), Dkt.Ng’wanza Kamata (Mwenye miwani) na
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Bi.Latifa Khamis (wa pili kulia)
alipotembelea Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba
yanayofanyika katika uwanja vya Mwl. Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam
ambapo tarehe 03 Julai Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa atayafungua
rasmi.
Na.Mwandishi Wetu-MAELEZO
Serikali
imewataka Wananchi kuendelea kupenda bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya hapa
nchini kwani chanzo cha nchi kufikia uchumi wa kati ni pamoja na wananchi wake
kupendelea bidhaa ambazo wanazizalisha wao kama wao, na mafanikio yametokana na
juhudi za watanzania wote wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dkt.John Pombe Magufuli.
Akizungumza
baada ya kutembelea mabanda ya maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa (sabasaba)
yanayofanyika katika Uiwanja vya Mwl.
Nyerere Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Innocent
Bashungwa amesema kuwa ili watanzania waweza kusheherekea mafanikio endelevu ya
kuingia nchi zenye kipato cha kati wanatakiwa kuwa wa kwanza kutangaza bidhaa zao.
"Kupitia
mafanikio tuliyoyapata rai yangu kwa watanzania ni kupenda bidhaa
zinazozalishwa na viwanda vyetu ili mafanikio haya ya nchi kuwa kwenye orodha
ya nchi zenye kipato cha kati yawe ni matunda kwa watanzania hasa kwa wakina
mama na vijana wanaotafuta ajira na
tukiendelea kupenda bidhaa zinazozalishwa hapa nchini ndivyo tunazidi
kutengeneza fursa za ajira kwa watanzania". Alisema Mhe.Bashungwa.
Alisisitiza
kuwa watanzania wanatakiwa kuangalia bidhaa za ndani Kabla hawajanunua bidhaa
kutoka nje ili kuweza kukuza viwanda na kuwa na uchumi wenye kipato cha kati
endelevu kwani ili Watanzania waendelea kusheherekea mafanikio haya ya kufikia
kipato cha kati tunatakiwa kupenda bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.
Alibainisha
kuwa kupitia maonesho 44 ya Biashara kimataifa (sabasaba) ambapo takribani kampuni mbalimbali ndani na nje ya nchi
zitashiriki, kutakuwa na fursa ya wananchi kuja kununua bidhaa na kuangalia
teknolojia mbalimbali zikioneshwa na taasisi na makampuni ya kitanzania, pia kupitia B2B wale ambao wapo nje
wataendelea kuingia mikataba na wafanyabiashara ambao wanashiriki katika
maonesho ya sabasaba hayo.
Pamoja
na hayo Mhe. Bashungwa amesema Tanzania kuwa nchi yenye kipato cha kati
inasaidia kuingia kwenye rada ya kimataifa hivyo wengi watapenda kuja kuwekeza
hapa nchini.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent
Bashungwa, akipata maelezo kutoka kwa Afisa wa Shirika la Viwango Tanzania
(TBS), alipotembelea banda hilo katika Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa
maarufu kama Sabasaba yanayofanyika katika uwanja vya Mwl. Julius Nyerere,
Jijini Dar es Salaam ambapo tarehe 03 Julai Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe Kassim
Majaliwa atayafungua rasmi
Waziri
wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa, akipata maelezo kutoka kwa
Afisa wa Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA),alipotembelea banda hilo
katika Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba
yanayofanyika katika uwanja vya Mwl. Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam
ambapo tarehe 03 Julai Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa atayafungua
rasmi.
Waziri
wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa, akiangalia bidhaa kutoka kiwanda cha kutengeneza vifaa vya Umeme
cha AfriCAB alipotembelea banda hilo katika Maonesho ya 44 ya Biashara ya
Kimataifa maarufu kama Sabasaba yanayofanyika katika uwanja vya Mwl. Julius
Nyerere, Jijini Dar es Salaam ambapo tarehe 03 Julai Waziri Mkuu wa Tanzania,
Mhe Kassim Majaliwa atayafungua rasmi.
Waziri
wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa, akiangalia bidhaa kutoka kiwanda cha kutengeneza vifaa vya Umeme
cha AfriCAB alipotembelea banda hilo katika Maonesho ya 44 ya Biashara ya
Kimataifa maarufu kama Sabasaba yanayofanyika katika uwanja vya Mwl. Julius
Nyerere, Jijini Dar es Salaam ambapo tarehe 03 Julai Waziri Mkuu wa Tanzania,
Mhe Kassim Majaliwa atayafungua rasmi.
Waziri
wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa, akiangalia bidhaa kutoka kwa wajasiriamali wanaofadhiliwa na
Benki ya Biashara Tanzania (NBC), alipotembelea banda hilo katika Maonesho ya
44 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba yanayofanyika katika uwanja
vya Mwl. Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam ambapo tarehe 03 Julai Waziri
Mkuu wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa atayafungua rasmi.
Waziri
wa Viwanda na Biashara, Mhe. Innocent Bashungwa, akiangalia bidhaa kutoka kwa wajasiriamali wanaofadhiliwa na
Benki ya Biashara Tanzania (NBC), alipotembelea banda hilo katika Maonesho ya
44 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba yanayofanyika katika uwanja
vya Mwl. Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam ambapo tarehe 03 Julai Waziri
Mkuu wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa atayafungua rasmi.
No comments:
Post a Comment