Naibu Waziri Ofisi ya
Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima akitoa maelekezo kwa Bw
Honest Mrema Meneja Mkuu wa Mgodi wa Shanta mara baaada ya Naibu Waziri Sima
kutembelea mgodi huo kukagua bwawa la kuhifadhi tope sumu litokanalo na
uchenjuaji wa dhahabu mgodini hapo.
Na
Lulu Mussa -Songwe.
Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima ameuagiza uongozi wa
Wilaya ya Songwe kuwabaini, kuwasajili na kuunda vikundi vya wachimbaji wadogo
wasio rasmi ili waweze kutambulika na kufaidika na mikopo midogo midogo
inayotolewa na Serikali hapa nchini.
Ameyasema hayo hii leo
mara baada ya kufanya ziara ya kikazi katika Mkoa wa Songwe hususan Wilaya ya
Songwe na kubaini changamoto ya wachimbaji wadogo wanaoharibu mazingira
kutokana na uchimbaji holela.
“Ni lazima mchukue hatua
za haraka za kuwatambua wachimbaji hawa kwa lengo la kuwasajili na kuanzisha kanzi
data itakayosaidia katika zoezi la utoaji wa elimu ili kunusuru mazingira” Sima
alisisitiza.
Waziri Sima amesisitiza
kuwa ni vema pia Wilaya ya Songwe ikaanzisha vikundi vya mazingira na
kuhamasisha matumizi ya Sheria ndogondogo katika maeneo yao.
Akiwasilisha taarifa ya
hali ya Mazingira katika Wilaya hiyo Mkuu wa Wilaya ya Samuel Jeremia Opulukwa
amesema Wilaya yake inakabiliwa na changamoto kubwa za uchomaji wa misitu
unaohatarisha maisha ya viumbe hai na ikolojia ya eneo hilo.
Katika hatua nyingine
Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)
Dkt. Samuel Gwamaka ametoa wito kwa watafiti wa madini katika eneo hilo kutoa
taarifa rasmi katika ngazi ya Wilaya ili kuepuka uharibifu wa mazingira
unaofanywa na watafiti hao kwa kuchimba kiholela kwa lengo la kutafuta dhahabu.
Pia, Naibu Waziri Sima
ametembelea Mgodi wa Shanta na kuagiza uongozi wa mgodi huo kutoa elimu kwa
jamii inayozunguka mgodi huo juu ya namna bora ya uchimbaji wa madini kwa njia
bora na salama kwa mazingira.
“Kwa kuwa mgodi huu
unatumia teknolojia ya kisasa zaidi, natoa rai kwa mgodi kuhamisha teknolojia
hii kwa wachimbaji wadogo wadogo ili wananchi pia wanufaike” Sima alisisitiza.
Mheshimiwa Mussa Sima yuko
Mkoani Songwe kwa ziara ya kikazi na ametembelea Wilaya ya Songwe na kukagua
usimamizi na uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira ambapo kesho atawasili Mkoani
Mbeya.
Naibu Waziri Ofisi ya
Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima akitoa maelekezo kwa Bw
Honest Mrema Meneja Mkuu wa Mgodi wa Shanta mara baaada ya Naibu Waziri Sima
kutembelea mgodi huo kukagua bwawa la kuhifadhi tope sumu litokanalo na
uchenjuaji wa dhahabu mgodini hapo.
Dkt. Samuel Gwamaka
Mkurugenzi Mkuu, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira – NEMC
akisalimiana na baadhi ya watumishi wa mgodi wa Shanta Gold Wilayani Songwe
akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira ya
Mwaka 2004.
Naibu Waziri Ofisi ya
Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima akiongea na Mkuu wa Wilaya
ya Songwe Bw. Samuel Jeremia Opulukwa (wa pili kushoto) wakati wa ziara ya
kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi wa Mazingira katika Wilaya hiyo. Kulia
ni Prof Esnat Chaggu Mwenyekiti wa Bodi – Baraza la Taifa la Hifadhi na
Usimamizi wa Mazingira NEMC na Dkt. Samuel Gwamaka Mkurugenzi Mkuu – NEMC.
Prof Esnat Chaggu
Mwenyekiti wa Bodi – Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC
akisisitiza jambo mara baada ya kufanya ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za
uhifadhi wa Mazingira katika Wilaya ya Songwe hii leo.
No comments:
Post a Comment