Na Jaala Makame Haji
Tume ya Uchaguzi ya Zanziba ZEC imewataka wasimamizi wa Uchaguzi wa Wilaya
kuwa makini na kuvipitia
vipengele vya Sheria ya Uchaguzi
no 4 ya mwaka 2018 na kanuni za
uchaguzi za mwaka 2020 ambazo zitawapatia maelekezo
mazuri ya kutekeleza majukumu yao katika kusimamia uchaguzi mkuu 2020
Makamo
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ZEC MABRUK
JABU MAKAME akizugumza wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa
wasimamizi na Wasimamizi wasaidizi wa
Wilaya 11 za Zanzibar alisema shughuli
za Uchaguzi Mkuu zinahitaji kuendeshwa kwa kufuata
misingi ya Katiba, Sheria
na Kanuni za Uchaguzi ili kila mwenye haki aweze kuipata fursa hiyo.
“waelekezeni
vizuri juu ya utaratibu wa kisheria wateuliwa hao bila ya kujali ni nani
amefika katika Ofisi yako kupata huduma” alisema
Alifafanua
kuwa, mbali ya kuwepo kwa mafanikio makubwa
katika kuendesha kazi za Uchaguzi
katika hatua mbali mbali ikiwemo kazi ya Mapitio ya Majimbo ya Uchaguzi ambapo
kwa sasa ni 50 badala ya 54,
uandikishaji wa wapiga kura wapya
na uhakiki wa taarifa za wapiga kura , utoaji wa vitambulisho vya Kupigia Kura
lakini pia wanapaswa kuwa makini na waangalifu
zaidi katika kazi ya utoaji wa fomu za uteuzi wa Wagombea
Hata hivyo, aliwasisitiza wasimamizi hao kuhakikisha
wanafatilia kwa ukaribu kazi
ya upigaji kura , kuhesabu na kujumlisha
kura katika vituo na majimbo
wanayo yasimamia.
Mkurugenzi
wa Uchaguzi THABIT IDAROUS FAINA alisema madhumuni ya Tume katika kuwapatia
mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao katika Uchaguzi Mkuu
2020.
Akiwasilisha
mada kuhusu kampeni za Wagombea Mkuu wa Kurugenzi ya Rasilimali Watu, Mipango
na Uendeshaji wa ZEC SAADUN AHMED KHAMIS alisisitiza kwamba, Msimamizi wa
Uchaguzi ahakikishe Mikutano yote ya kampeni za Uchaguzi katika Wilaya yake
inaendeshwa katika muda na maeneo yaliyoainishwa kisheria.
Mafunzo
kwa Wasimamizi na Wasimazi wa Uchaguzi wa Wilaya yanaendelea kufanyika ikiwa hatua
ya utekelezaji wa mpangokazi wa uchaguzi wa kuwapatia mafunzo watendaji wote
watakao husika na kazi ya usimamizi wa Uchaguzi
No comments:
Post a Comment