Dar es Salaam, TANZANIA. Hapo tarehe 15 Oktoba,
2020 Balozi wa Marekani nchini Tanzania Dk. Donald J. Wright, katika hafla
iliyofanyika katika makazi yake jijini Dar es Salaam,alitoa ruzuku kwa asasi za
kiraia, taasisi zisizojiendesha kibiashara na taasisi za kidini zilizosajiliwa
zipatazo 13 kutoka pande zote za Tanzania. Ruzuku huyo ilitolewa kutoka katika
Mfuko wa Balozi wa Marekani wa Kusaidia Mapambano Dhidi ya Ukimwi (AFHR) ili
kutekeleza miradi ya kukabiliana na VVU nchini.
Fedha zinazotolewa na mfuko huu hutolewa na Mpango wa
Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR), ambao
unawasilisha ahadi na dhamira ya dhati ya Serikali ya Marekani ya kukabiliana
na janga la VVU/UKIMWI. Mpango huu bado
unaendelea kuwa mpango mkubwa zaidi kuwahi kutekelezwa na nchi yoyote duniania
katika kukabili ugonjwa wa aina moja.Toka kuanzishwa kwa PEPFAR hapo mwaka
2003, Serikali ya Marekani imechangia zaidi ya Dola za Kimarekani milioni 4.6 kukabiliana
na VVU nchini Tanzania pekee.
Wapokea ruzuku waliwasilisha maombi na maandiko yao ya
miradi kushughulikia masuala mbalimbali yanayohusu VVU/UKIMWI katika jamii zao.
Miradi iliyopendekezwa ililenga kuongeza uelewa kuhusu VVU, kuimarisha upatikanaji
wa huduma miongoni mwa watu wanaoishi na VVU, yatima na watoto walio katika
mazingira hatarishi pamoja na makundi ya ya watu walio katika hatari zaidi ya
kuambukizwa ikiwemo wanaume na vijana wa kiume, wasichana na vijana wa kike.
Miradi iliyoshinda na kupatiwa ruzuku inalenga katika
vipaumbele vya kimkakati ikiwa ni pamoja na kuinua ufahamu kuhusu tiba miongoni
mwa watu wanaoishi na VVU; kupunguza unyanyapaa na ubaguzi; mbinu bunifu za
kupunguza ukatili wa kijinsia na upatikanaji wa huduma kwa wahanga wa vitendo
vya ukatili wa kijinsia; kuwafikia na kuwahimiza wanaume kupima VVU na
kuwaunganisha na huduma za matibabu; na kuinua ubora wa huduma za kukabiliana
na VVU kwa kupitia ufuatiliaji unaoendeshwa na jamii (community-led monitoring).
Toka kuanzishwa kwake mwaka 2009,Mfuko wa Balozi wa
Kukabiliana na VVU/UKIMWI (AFHR) umeshatoa ruzuku kwa asasi za kijamii ma
taasisi za kiraia zipatazo 130 nchini Tanzania. Marekani ina fahari kuendelea
kuwa mbia imara wa asasi na taasisi hizi ili kufikia malengo ya Tanzania ya
kudhibiti VVU.
Kwa
taarifa zaidi, tafadhali wasiliana na Kitengo cha Habari cha Ubalozi wa
Marekani Dar es Salaam kwa simu: +255 22 229-4000 au barua pepe: DPO@state.gov.
Wapokea
Ruzuku kutoka katika Mfuko wa Balozi wa Kukabiliana na VVU/UKIMWI kwa mwaka 2020:
1.
Mpango wa Taifa wa
Kudhibiti UKIMWI wa BAKWATA utashughulikia vikwazo mbalimbali
vinavyowafanya watu wanaoishi na VVU kuacha kuendelea kutumia dawa (ARVs) kwa
kuimarisha mitandao ya watu wanaoishi na VVU kupitia waelimisha rika (peer
educators) kwa ushirikiano na wahudumu wa afya katika wilaya ya Uvinza, mkoani
Kigoma.
2.
Chimaba Sanaa itaimarisha uelewa
kuhusu matibabu kwa kutumia dawa za kufubaza VVU (ARVs) na kuongeza kiwango cha
wanaume na vijana wa kiume wanaoishi na VVU, pamoja na wenza wao kutumia dawa
hizo bila kukoma katika wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya.
3.
Development for All
(DEFOA)itainua ubora wa huduma kwa watu wanaoishi na VVU wanaopatiwa dawa za
kufubaza VVU (ARVs) katika vituo vya afya kwa kupitia watoa huduma za afya
ndani ya jamii (Community
health workers) na walengwa wenyewe.
4.
Foster Community
Creative Solutions (FCCS) itaongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kupima VVU; kuanza
matibabu ya dawa za Kufubaza VVU (ART) kwa kutumia dawa mchanganyiko za TLD miongoni mwa wakulima wadogo
wadogo na wafugaji na kuinua ujuzi wa kutoa matibabu yanayohusisha dawa za
kufubaza VVU miongoni mwa Watoa Huduma za Afya wa Jamii katika Halmashauri ya
Wilaya ya Bahi.
5. Katandala HIV/AIDS Free Club (KFC) itafuatilia ili kuboresha huduma zitolewazo kwa
watu waishio na VVU wanaopa dawa za kufubaza VVU (ARVs) katika Kituo cha Afya
cha Usevya kwa kutumia mbinu ya
kuishirikisha jamii katika kutathmini huduma zitolewazo (community score card
approach).
6. Kilio cha Waathirikana Waathiriwa UKIMWI Tanzania (KIWWAUTA)itapunguza kiwango maambukizi mapya
kwa makundi ya watu walio katika hatari zaidi ya kupata maambukizi ya VVU.
7. Participatory Development Concern (PADECO)itafuatilia ili kuboresha huduma
zitolewazo kwa watu waishio na VVU wanaopa dawa za kufubaza VVU (ARVs) katika
Kituo cha Afya kwa kutumia mbinu ya kuishirikisha jamii katika kutathmini
huduma zitolewazo (community score card approach).
8. Social Action Trust fund (SATF)itaboresha maisha ya yatima na watoto walio katika
mazingira hatarishi pamoja na walezi wao na kuwezesha upatikanaji wa huduma
bora kwao kwa kuwajengea uwezo na kufanya ushawishi.
9. SHDEPHA+ MPANDAitaongeza
idadi ya watu wazima na vijana wa kiume walio katika hatari ya maambukizi ya
VVU wanaojua hali zao za kiafya kuhusu maambukizi ya VVU kwa kuendesha upimaji
wa VVU katika maeneo yenye kiwango kikubwa cha maambukizi lakini yasiyopata
huduma za kutosha katika mkoa Katavi.
10. Hospitali Teule ya Wilaya ya SUMVE itatoa elimu ya VVU/UKIMWI kuhusu matibabu kwa kutumia
dawa za kufubaza VVU, matumizi ya dawa mseto ya Tenofovir, Lamivudine,
na Dolutegravir (TLD) na ngono salama kwa vijana wa kuanzia umri wa miaka 15
-24 katika mashule, vituo vya afya na jamii kwa ujumla.
11. Tanzania Health Promotion Support (THPS)itaboresha huduma za kukabiliana na
ukatili wa kijinsia kwa jamii na kuboresha huduma za kinga na matibabu katika
vituo vya afya katika wilaya ya Mkuranga, Mkoani Pwani.
12. Umbrella of Women and Disabled Organization (UWODO)itaimarisha upatikanaji wa huduma za
upimaji wa VVU kwa wanawake, wasichana na watu wenye ulemavu katika wilaya ya
Makambako Mjini, na kuhakikisha kuwa makundi hayo yanapewa elimu kuhusu huduma
za matibabu pamoja na kuunganishwa na huduma hizo.
13. Tanzania Youth Behavior Change Organisation (TAYOBECO) itajenga uelewa kuhusu matumizi ya
dawa mchanganyiko ya Tenofovir, Lamivudine, na Dolutegravir (TLD) kama
tiba ya mwanzo inayopendekezwa wa watumiaji wa ARV na kukufa ufahamu kuhusu
tiba inayopendekezwa sasa kwa kuzingatia miongozo ya utoaji huduma ya dawa za
kufubaza makali ya VVU kwa makundi yaliyo katika hatari zaidi ya kuambukizewa
VVU katika wilaya 5 za mkoa wa Dar
es salaam.
Kufahamu zaidi
kuhusu Mfuko wa Balozi wa Kukabiliana na VVU/UKIMWI, tafadhali tembelea tovuti
ya PEPFAR
Tanzania (https://tz.usembassy.gov/our-relationship/pepfar/) au wasiliana na Mratibu wa PEPFAR
anayeshughulikia Asasi za Kiraia (Civil Society Outreach Coordinator) kwa barua
pepe: PEPFARGrantsDar@state.gov
No comments:
Post a Comment