STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar
07.12.2020
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Hussein Ali Mwinyi amemteua Maalim Seif Sharif Hamad kuwa Makamo wa Kwanza wa Rais
wa Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa
kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu
Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, uteuzi huo umeanza jana tarehe 6 Disemba,
2020.
Aidha, taarifa hiyo
ilieleza kwamba kwa kuzingatia matakwa ya Kifungu cha 9(3) cha Katiba ya
Zanzibar ya mwaka 1984, kinachosema kwamba “Muundo wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar utakuwa wa Umoja wa Kitaifa na utendaji wa kazi zake utafanywa katika
utaratibu utakaohakikisha kuendelezwa kwa umoja nchini na lengo la kufikia
demokrasia”.
Hatua hiyo imekuja
baada ya Chama cha upinzani cha ACT Wazalendo kuafikia uamuzi wa kujiunga na
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Awamu ya Nane itakayokuwa na Muundo wa
Serikali ya Umoja wa Kitaifa inayoongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi.
Katibu Mkuu wa chama
hicho cha ACT Wazalendo Ado Shaibu akizungumza na waandishi wa habari hapo jana
tarehe 6 Disemba, 2020 huko Jijini Dar-es Salaam alisema kuwa katika mkutano
maalum wa Kamati Kuu ya chama hicho wameamua kupendekeza jina la mwanachama
atakayekuwa Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Sambamba na hayo,
chama hicho pia, kimeruhusu Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Wabunge, na
Madiwani waliochaguliwa kukiwakilisha chama hicho na wananchi waliowachangua
kushiriki kikamilifu katika nafasi zao walizochaguliwa.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment