Na Beatrice Sanga, MAELEZO
Wakati
Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ikiadhimisha miaka 40
tangu kuanzishwa kwake, Tanzania ikiwa ni sehemu ya umoja huo inajivunia mambo
mbalimbali ikiwepo Kiswahili kutumika kama miongomi mwa lugha kuu za
mawasiliano kwa viongozi Wakuu na Mawaziri wa Nchi hizo
Akizungumza
na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam wakati wa Mkutano wa Baraza la
Mawaziri wa jumuiya hiyo, Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuingia kwa Kiswahili katika SADC
ni uamuzi uliofanywa katika kikao cha 39 cha wakuu wa nchi hizo
“katika kikao cha 39 cha wakuu wa Nchi wa SADC
iliamuriwa Kiswahili iwe ni lugha ya nne ya SADC na kitumike katika mikutano ya
baraza la mawaziri na mkutano wa wakuu wa nchi, lakini sasa imeamuliwa
Kiswahili kitatumika sio tu katika
mikutano hiyo miwili lakini katika mikutano yote ya kisekta yani mikutano ya
sekta ya Afya, sekta ya elimu, sekta ya uchukuzi, kwahiyo sasa Kiswahili
kitatumika pia katika ngazi ya sekta ambayo ni hatua kubwa iliyofikiwa”,
amesema Prof. Kabudi.
Aidha
prof kabudi amesema katika kikao chao cha Baraza la Mawaziri wa Jumuiya hiyo
kinachoendelea kwa njia ya mtandao watajadili na kukamilisha mchakato wa
utengenezaji wa Sanamu maalumu ya Baba wa Taifa mwalimu Julius Kambarage
Nyerere ambayo itawekwa katika Jengo la Amani kwenye makao makuu ya Umoja huo
Mjini Addis Ababa Nchini Ethiopia ikiwa
ni maamuzi yaliyofanywa na SADC
takribani miaka miwili iliyopita
“kwa miaka takribani miwili sasa,Jumuiya ya SADC iliamua kutengeneza sanamu maalumu ya baba wa Taifa mwalimu Julius kambarage nyerere ambayo itawekwa jengo la Amani, kule Addis Ababa Ethiopia, mchakato unaendelea na tunaamini katika kikao hichi tutakamilisha mchakato wa kumpata mtu atakayeifua hiyo sanamu ya mwalimu Julius kambarage nyerere,” amesema Prof Kabudi.
No comments:
Post a Comment