Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP Simon Sirro akizindua Kitabu cha muongozo wa kufichua na kuzuia uhalifu kitabu ambacho kinalenga kutoa dira hasa katika utekelezaji wa mpango wa Polisi kata kupitia mpango mkakati wa ushirikishwaji wa jamii.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewataka watu wanaopata
msamaha wa vifungo kutoka gerezani kuacha kujihusisha na uvunjifu wa amani
ikiwa pamoja na kuacha kujiingiza tena kwenye matukio ya uhalifu na badala yake
wajikite katika kuleta maendeleo kwenye jamii.
IGP Sirro amesema hayo leo wakati akizindua kitabu cha muongozo wa
kufichua na kuzuia uhalifu kitabu ambacho kinalenga kutoa dira hasa katika
utekelezaji wa mpango wa Polisi kata kupitia mpango mkakati wa ushirikishwaji
wa jamii.
No comments:
Post a Comment