Habari za Punde

Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa Ameshiriki Droo ya Kukutanisha Timu kwa Ajili ya Robo Fainali Michuano ya Jimbo Cup.

Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akimkabidhi jezi Kapteni wa timu ya Chinokole FC, Abdallah Suleiman, wakati wa droo ya kukutanisha timu kwa ajili ya robo fainali, katikati ni Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Ruangwa Yusuf Mpame.
Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akisaini mpira baada ya kufanyika kwa droo ya kukutanisha timu kwa ajili ya robo fainali ya Jimbo Cup kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Ruangwa Yusuf Mpame.
Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akimkabidhi mpira Kapteni wa timu ya Taifa Jipya FC, Said Mtalimbo, wakati wa droo ya kukutanisha timu kwa ajili ya robo fainali, katikati ni Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Ruangwa Yusuf Mpame
Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akimkabidhi kombe kwa ajili michuano ya Jimbo Cup Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa miguu Wilaya ya Ruangwa Yusuf Mpame, wakati wa droo ya kukutanisha timu kwa ajili ya robo fainali, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Hassan Ngoma.
Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa soka Wilaya ya Ruangwa na makapteni wa timu zinazoshiriki Jimbo Cup, wakati wa droo ya kukutanisha timu kwa ajili ya robo fainali, Agosti 19,2021 
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.