Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Geoffrey Mwambe (kulia) na Rais wa Dkt.Hossam Darwish wa Jumuiya ya Muungano Kimataifa chini ya kundi la Afrika na Asia (Afro-Asian Union (AFASU) wakisaini makubaliano ya Ushirikiano wa Tanzania na Jumuhiya ya wafanyabiashara kutoka nchini Misri . Makubaliano hayo yanalenga kuhamasisha na kuendeleza masuala ya biashara, uwekezaji na Utalii katika sekta za Kilimo, Viwanda, Biashara mtandao, Utalii, Elimu na TEHAMA, leo tarehe 12 Oktoba, 2021.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Geoffrey Mwambe, na Rais wa Dkt.Hossam Darwish wa Jumuiya ya Muungano Kimataifa chini ya kundi la Afrika na Asia (Afro-Asian Union (AFASU) wakiwa na watendaji kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) na Kituo cha Uwekezaji Tanzania, baada ya kuingia makubaliano ya Ushirikiano na Jumuiya ya wafanyabiashara ya AFASU, yaliyoingiwa na Serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji, kwa ajili ya kuendeleza na kuhamasihsa uwekezaji nchini, leo tarehe 12 Oktoba, 2021.
Baadhi ya maafisa wa serikali kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Misri, Wizara ya mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Mkurugenzi Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), wakifuatailia utiaji Saini wa makubaliano ya Ushirikiano na wafanyabiashara kutoka nchini Misri kupitia Jumuiya ya Muungano Kimataifa chini ya kundi la Afrika na Asia (Afro-Asian Union (AFASU) yaliyoingiwa na Serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji, leo tarehe 12 Oktoba, 2021
Na. Beatrice Sanga - MAELEZO
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Geoffrey Mwambe Pamoja na Raisi wa Jumuiya
ya Muungano Kimataifa chini ya kundi la Afrika na Asia (Afro- Asian union
(AFASU) Dr. Hossam Darwish wametia saini hati ya makubaliano ya kujumuika, kukuza na kuunda ushirikiano katika
sekta ya uwekezaji (MoU) wenye lengo la
kuwezesha na kukuza uwekezaji, biashara na utalii nchini Tanzania .
Akizungumza
katika hafla ya utiaji saini makubaliano hayo iliyofanyika katika Ofisi Ndogo
ya Waziri Mkuu Jijini Dar es salaam, Mhe. Mwambe ameainisha maeneo ambayo
Tanzania na ASAFU watashirikiana katika kuvutia maeneo ya uwekezaji kuwa ni
pamoja na uwekezaji katika kilimo, Viwanda, Biashara ya Kielektroniki, Utalii,
elimu pamoja na Uwekezaji katika ICT na uanzishaji wa elektroniki.
Mhe.
Mwambe ameeleza kuwa kusainiwa kwa hati ya makubaliano kunaonyesha dhamira
kubwa ya serikali ya awamu ya sita ya
kushirikiana na wadau wote duniani na kuwaalika katika uwekezaji lakini pia
kutumia fursa ya kuaminika kama serikali ya Tanzania kuweza kuwaomba Taasisi
na sekta binafsi waweze kutusemea
ili kushawishiana kuja kuwekeza Tanzania kwasababu ya mazingira bora ya
uwekezaji yaliyowekwa nchini.
“Serikali
ya awamu ya sita inaaminika na mazingira
ya uwekezaji Tanzania yameendelea kuboreshwa
na pia sisi kwenye Nyanja za
kimataifa tafsiri yake ni kuwa tanzania
inaendelea kusifika kwenye ubora wake wa mazingira ya uwekezaji”Amesema
Mhe. Mwambe
Aidha
Mwambe amewashukuru wawekezaji hao na kuwahakikishia kuwa ofisi yake iko tayari
kushirikiana nao kwa kuweka mazingira wezeshi ili kuhakikisha wanafanikiwa, na
kuwataka watanzania na Taasisi nyingine za serikali kuwapa ushirikiano wa kutosha ili waweze
kufanikiwa kuwekeza nchini.
“Nawashukuru
sana AFASU, nawakaribisha sana na ninawaomba watanzania tuendelee kuwapa
ushirikiano wote pale ambapo wataitaji vibali,
ardhi, na idhini mbalimbali za
serikali ili waweze kutekeleza mradi
wao tutahakikisha kwamba tunasimamia
hilo kwahiyo tusingependa kuwakwamisha kwa sababu hii inatupa sifa sisi na inampa pia amani Mhe. Rais na kuendelea
kujenga imani kubwa kwa wawekezaji wa
ndani na nje ya nchi
Kwa
upande wake Rais wa Jumuiya hiyo, Dkt. Hossam Darwish amesema Jumuiya ya AFASU
wako tayari kutekeleza vipengele vyote ambavyo
vimo ndani ya makubaliano hayo na
watatekeleza kwa nguvu kubwa na haswa
kwa kuanza na sekta ya kilimo ambapo
ndani ya Jumuiya wanao wajumbe
ambao ni
wawekezaji wakubwa kwenye sekta ya kilimo ambapo wameona maeneo ya kilimo na wamevutiwa sana na fursa hiyo ya kilimo hapa nchini na hivyo
wanatoa ishara njema kwamba wao
watakuwa ni sehemu ya uwekezaji katika sekta hii ya kilimo pamoja na sekta nyingine ambazo zitakuwa
zimeainishwa katika makubaliano.
Dkt.
Hossam ameongeza kuwa kwa hatua ya
kwanza na kwa haraka wataanza na mradi
wa chuo cha Kimataifa cha Kitanzania cha mifumo ya kielektroniki ambacho kitakuwa
na vitivo mbalimbali vya kimasomo ya kielimu
na wanaimani kwamba vitivo hivyo
vinaweza kwenda sambamba na kile
walichokiona kinahitajika ndani ya nchi yetu
ambapo shahada mbalimbali zitatolewa kupitia chuo hicho na kitaweza
kuchukua wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali za Afrika nakuhakikisha kuwa mfumo
wa masomo utaweza kutoa wataalamu wa kutosha.
Amesema
hatua nyingine itakayofuata ni mradi wa maonyesho ya biashara ambayo
yatafanyika hapa nchini Tanzania ili kuweza kuchochea uwekezaji na pia jumuiya
hiyo itajikita katika uwekezaji wa masuala ya utalii hususan katika ujenzi wa
hoteli zenye hadhi kubwa na katika sekta ya afya watajikita katika ujenzi wa
viwanda vya kuzalisha Dawa na vifaa Tiba .
Kwa
upande mwingine Dkt. Hossam amemshukuru Waziri wa Uwekezaji kwa kuonesha uzalendo mkubwa kwa nchi yake ambapo
amekuwa na juhudi kubwa sana na kwa
upande wake anamatumaini makubwa kuwa Tanzania itapiga hatua katika sekta hii
ya uwekezaji kwa juhudi kubwa ambazo anazifanya Waziri wa Uwekezaji.
No comments:
Post a Comment