Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi Amewaapisha Wajumbe wa Tume ya Mipango Ikulu Zanzibar leo 27-12-2021.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Dk. Rahma Salim Mahfoudh kuwa Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar.hafla hiyo iliyofanyika leo 27-12-2021, katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewaapisha Wajumbe wapya wa Tume ya Mipango ya Zanzibar.

Hafla hiyo imefanyika leo Ikulu Jijini Zanzibar ikiwa ni kikao cha kwanza cha Tume hiyo katika Awamu ya Nane ya uongozi wa Rais Dk. Mwinyi ambapo Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Othman Masoud Othman  na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdullah walishiriki ikiwa ni Wajumbe kutokana na vyeo vyao.

Mara  baada ya kiapo hicho, Rais Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo kuwapongeza Wajumbe hao wapya aliowaapisha pamoja na wale wa zamani wanaoendelea.

Katika pongezi hizo, Rais Dk. Mwinyi alieleza matumaini yake makubwa kwa wajumbe hao wa Tume ya Mipango ya Zanzibar katika kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Wajumbe walioapishwa ni Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar  Dk. Mwinyi Talib Haji,Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Mhe.Jamal Kassim Ali, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Mhe.Riziki Pembe Juma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Kazi, Uchumi na Uwekezaji Mhe.Mudrik Ramadhan Soraga.

Wengine ni Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe.Omar Said Shaaban,Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Mhe.Rahma Kassim Ali, Waziri wa Maji, Nishati na Madini Mhe.Suleiman Masoud Makame,Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mhe.Lela Muhamed Mussa, Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Mhe.Abdalla Hussein Kombo pamoja na  Dk. Rahma Salim Mahfoudh Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar.

Wajumbe hao wapya walioapishwa hivi leo waliahidi kutekeleza majukumu yao kwa maslahi na uchumi wa Zanzibar.

Nao wajumbe wa zamani wa Tume hiyo ya Mipango ya Zanzibar Mohammed Faki Mohammed pamoja na Profesa  Semboja Haji Hatib walitoa shukurani zao kwa Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi kwa kuendelea kuwaamini kuwa Wajumbe wa Tume hiyo na kuahidi kwamba wataendelea kufanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya Zanzibar.

Imetayarishwa na Kitengo cha Habari.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said, kuwa Mjumbe mpya wa Tume ya Mipango Zanzibar, hafla hiyo iliyofanyika leo 27-12-2021, katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mhe.Dkt. Mwinyi Talib Haji, kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango Zanzibar, hafla hiyo iliyofanyika leo 27-12-2021, katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar.Mhe Jamal Kassim Ali,kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango Zanzibar,hafla hiyo iliyofanyika leo 27-12-2021, katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisaini hati ya Kiapo ya Waziri wa Ardhi, Maendeleo na Makaazi Zanzibar Mhe.Riziki Pembe Juma, baada ya kumuapisha kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi Uchumi na Uwekezaji Zanzibar Mhe Mudrik Ramadhani Soraga, kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Mhe Omar Said Shaban, kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Zanzibar Mhe. Rahma Kassim Ali, kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 27-12-2021 Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Waziri wa Maji Nishati na Madini Zanzibar Mhe.Suleiman Masoud  kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 27-12-2021 Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe.lela Mohammed Mussa, kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 27-12-2021 Jijini Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Waziri wa Uchumu wa Buluu na Uvuvi Zanzibar Mhe. Abdalla Hussein Kombo,kuwa Mjumbe wa Tume ya Mipango, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 27-12-2021 Jijini Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.