Habari za Punde

Wanufaika Mikopo ya Elimu ya Juu Wajitokeza Kulipa Madeni Yao Mkoani Tanga.

.    Afisa Mikopo Mwandamizi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Sophia Saidan akitoa huduma kwa wateja mbalimbali waliotembelea Banda la HESLB leo  Jumapili (Machi 13, 2022) Mkoani Tanga wakati wa kampeni ya SIFURISHA inayoendelea katika Ofisi za Halmashauri ya Jiji la Tanga. Kampeni hiyo inalenga kuhumasisha urejeshaji wa mikopo ya elimu ya juu kutoka kwa wanufaika.

 Maafisa Mikopo wa HESLB wakitoa huduma mbalimbali kwa wateja leo Jumapili Machi 13, 2022 Mkoani Tanga wakati wa Kampeni ya SIFURISHA inayolenga kuhamasisha urejeshaji wa mikopo ya elimu ya juu inayoendelea katika Ofisi za Halmashauri ya Jiji la Tanga.

1.  Meneja wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Ofisi ya Arusha, PatricK Shoo akimkabidhi barua ya kumaliza deni la Mkopo wa elimu ya juu TZS 11,345,845.20/- Milioni leo Jumapili (Machi 13, 2022) Mkoani Tanga, Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Handeni, Mhe. Yusuph Abdallah wakati wa kampeni ya SIFURisha inayoendelea katika Ofisi ya Halmashauri ya Jiji la Tanga.

1.    Afisa Mikopo Mwandamizi wa HESLB, Sunday Charles akimkabidhi barua ya kumaliza deni la mkopo wa elimu ya juu, TZS 9,736,900.90 Milioni, mtumishi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Mary Siphaelly leo Jumapili (Machi 13, 2022) mara ya baada kulipa kiasi cha TZS 1,888,000/- Milioni  na kumaliza deni la mkopo huo wakati wa kampeni ya SIFURISHA inayoendelea katika Ofisi za Halmashauri ya Jiji la Tanga.

(PICHA NA HESLB)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.