RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiagana na Kiongozi wa Ujumbe wa Wafadhili kutoka Chuo Kikuu cha Hauklend kutoka Nchini Norway Bw.Trond Mohn, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 15-6-2022
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein
Ali Mwinyi ameupongeza utayari wa uongozi wa Hospitali ya Chuo Kikuu cha
Hauklend cha nchini Norway kujenga Hospitali ya kisasa ya maradhi ya moyo hapa
Zanzibar.
Rais Dk.
Mwinyi aliyasema hayo leo Ikulu Zanzibar wakati alipofanya mazungumzo na uongozi
wa Hospitali ya Chuo Kikuu cha Hauklend cha nchini Norway ambao ulimuhakikishia
Rais Dk. Miwnyi kwamba uko tayari kuanza ujenzi huo hivi karibuni.
Katika maelezo
yake Rais Dk. Mwinyi alieleza kwamba ujenzi wa Hospitali hiyo utasaidia kwa
kiasi kikubwa kutoa huduma za maradhi ya moyo hapa Zanzibar na kupunguza
kuwasafirisha nje ya nchi wagonjwa wenye maradhi hayo.
Rais Dk.
Mwinyi alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inathamini uhusiano na
ushirikiano kati yake na Hospitali ya Chuo Kikuu cha Haukland ambao ulianzishwa
tokea mwaka 2007 ambao umeweza kuzaa matunda na iko tayari kuuendeleza.
Aliongeza kuwa
ushirikiano huo umeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kuimarisha sekta ya afya
Unguja na Pemba ikiwa ni pamoja na kujenga majengo ya Hospitali kwa ajili ya
akina mama na watoto katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, kusaidia ujenzi na vifaa
katika hospitali ya Kidongo chekundu pamoja na kusaidia vifaa tiba kadhaa.
Aidha, Rais
Dk. Mwinyi alitoa shukurani kwa uongozi wa Hospitali hiyo kwa kuendelea
kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuanzisha na
kuendeleza miradi mbali mbali katika sekta ya afya ikiwa ni pamoja na
kuendeleza mafunzo kwa wauguzi na madaktari wazalendo sanjari na kubadilishana
uzoefu.
Rais Dk.
Mwinyi alieleza haja ya kuimarisha mifumo katika sekta ya afya hatua ambayo
itasaidia kwa kiasi kikubwa kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Nao uongozi wa
Wizara ya Afya ulieleza mahusiano na mashirikiano yaliopo kati ya Hospitali
hiyo na Hospitali ya Mnazi Mmoja huku uongozi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja
ukieleza mafanikio makubwa yatakayopatikana baada ya kukamilika na kuanza kazi
kwa Hospitali hiyo kutokana na maradhi ya moyo kuwa ni maradhi yalioshika kasi
hapa nchini na duniani kwa jumla.
Nao uongozi
huo wa Hospitali ya Chuo Kikuu cha Hauklend cha nchini Norway ulimueleza Rais
Dk. Mwinyi azma yao ya kujenga Hospitali kwa ajili ya kutoa huduma za maradhi
ya moyo hapa Zanzibar.
Katika maelezo
yao uongozi huo ulimuhakikishia Rais Dk. Mwinyi kwamba wako tayari kuanza
ujenzi huo ndani ya mwaka huu kwani wameshajipanga kuanza ujenzi wa mradi huo
mkubwa.
Pamoja na hayo,
uongozi huo ulisisitiza kwamba hatua hiyo ni miongoni mwa juhudi zao
wanazoendelea kuzichukua katika kuhakikisha wanaendeleza uhusiano na ushirikano
uliopo ambao umeanzishwa maalum kwa lengo la kuimarisha sekta ya afya hapa
Zanzibar.
Imetayarishwa na Idara ya Mawasiliano,
Ikulu Zanzibar. OF
RESPONSIBILITY
No comments:
Post a Comment