Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa mradi wa kuimarisha Elimu ya Sekondari wa
kuwajengea uwezo wa masomo ya Sayansi, Hisabati na Kiingereza walimu unakwenda
sambamba na mikakati ya Serikali ya kuhakikisha inatoa elimu bora inayoendana
na mahitaji ya sasa.
Rais
Dk. Mwinyi aliyasema hayo leo katika uzinduzi wa mafunzo ya Walimu wa Sayansi,
Hisabati na Kiingereza pamoja na makabidhiano ya Moduli na Miongozo ya Mafunzo,
hafla iliyofanyika huko katika hoteli ya Golden Tulip, iliyopo uwanja wa ndege
Zanzibar.
Katika
hotuba yake, Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa Elimu ya Sayansi na Hisabati ina
mchango mkubwa katika kufikia malengo hayo.
Alisema
kwamba ni dhahiri kuwa katika kufikia malengo hayo, ni lazima mikakati imara ya
kuinua ufaulu wa masomo ya Sayansi na Hisabati sambamba na uwezo katika lugha
ya Kiingereza kwa wanafunzi uimarishwe.
Aliongeza
kuwa katia kipindi cha miaka mitano iliyopita kuanzia mwaka 2017 hadi 2021,
matokeo ya wanafunzi katika mitihani ya Taifa ya kumaliza elimu ya Sekondari
hayakuwa yakiridhisha.
Alisema
kwamba kwa wastani asilimia 33 ya wanafunzi kila mwaka wanakosa vyeti na wengi
wao ni wale wanaosoma masomo ya Sayansi ambapo ufaulu mdogo wa wanafunzi hasa
katika masomo ya Sayansi na Hisabati unachangiwa kwa kiasi kikubwa na uhaba wa
walimu wenye sifa, uhaba wa maabara na uhaba wa vifaa vya kufundishia na
kujifunzia kwa vitendo.
Hivyo,
Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na washirika
mbali mbali wa maendeleo ili kuhakikisha changamoto zinazoathiri ufaulu wa
masomo ya Sayansi zinapatiwa ufumbuzi kwa kuwajengea walimu uwezo zaidi wa
ufundishaji wa masomo hayo na pia, kujenga maabara za Sayansi na kuzipatia vifaa.
“Nafurahi
kusikia kwamba tulianza kuwapatia mafunzo walimu 600 wanaosomesha Sekondari
Kidato cha Kwanza na cha Pili kwa masomo ya Sayansi, Hisabati na Kiingereza
kupitia Mradi wa ZISP ambao Serikali inautekeleza kwa ushirikiano na Benki ya
Dunia na leo tena kwa kushirikiana na KOICA tutawapatia mafunzo walimu wa Skuli
za Sekondari wa Kidato cha Tatu na cha Nne wanaosomesha masomo ya Sayansi,
Hisabati na Kiingereza Unguja na Pemba”,alisema Dk. Mwinyi.
Rais
Dk. Mwinyi alisema kuwa mkakati wa Serikali ni kuhakikisha Skuli zote mpya
zinakuwa na maabara za Sayansi, maabara za Kompyuta na maktaba za kisasa pamoja
na kuzipatia vifaa.
Alisema
kuwa hayo ni miongoni mwa mageuzi makubwa ya Elimu ambayo Serikali inaendelea
kuyafanyia kazi ambapo kupitia mageuzi hayo Serikali itaimarisha matumzi ya
Teknolojia katika Skuli zote ili kurahisisha ufundishaji na kujifunza kwa
walimu na wanafunzi hasa katika ngazi ya Elimu ya Msingi na Sekondari.
Rais
Dk. Mwinyi alisema kuwa matumizi ya Teknolojia yatawasaidia sana wanafunzi
kuweza kujifunza popote walipo na si lazima kuwepo darasani kwani itakumbukwa
wakati wa Janga la UVIKO-19, pale ambapo Skuli zilifungwa kwa takriban miezi
mitatu na bado wanafunzi waliendelea kusoma.
Alisisitiza
kwamba Serikali kupitia mageuzi ya Elimu itaimarisha mafunzo ya Amali na Ufundi
kwa kuhakikisha kila Wilaya ina vyuo vya aina hiyo kwa ajili ya watoto ili
waweze kupata ujuzi wa ufundi utakaowawezesha kujiajiri wenyewe na kujipatia
kipato kwa ajili ya kuimarisha maisha yao.
Rais
Dk. Miwnyi alitoa wito kwa walimu wote wa Skuli za Serikali, waliengwa wa
mafunzo hayo wanaofundisha masomo ya Hisabati, Sayansi na Kiingereza kushiriki
kikamilifu katika kuyapokea mafunzo hayo na kwenda kuyafanyia kazi wakati
wanapofundisha wanafunzi wao madarasani.
Sambamba
na hayo, Rais Dk. Mwinyi alilishukuru Shirika la Kimataifa la Maendeleo la
Korea washuku KOICA, ‘Good Neighbors’ na washirika wenzao wa maendeleo katika
kutekeleza na kufanikisha miradi huo muhimu wa mafunzo ya walimu aliyayazindua.
“Nawashukuru sana Serikali ya Korea ya Kusini, KOICA na Taasiasi ya Good
Neighbors’ kwa msaada wao huo mkubwa katika sekta ya elimu”,alisema Rais Dk.
Mwinyi.
Nae
Wazir wa Elimu na Mafunzo ya Amali Leila Mohammed Mussa alitoa pongeza kwa
KOICA kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katia kuimarisha sekta ya elimu.
Alieleza
kwamba mbali ya msaada wao huo wa mafunzo kwa walimu wa Sayansi wa Sekondari
pia, KOICA imesaidia katika ujenzi wa maabara kumi za kisasa ya Sayansi Unguja na Pemba.
Alieleza
juhudi za Serikali katika kuimarisha sekta ya elimu ambapo imetenga jumla ya
TZS Bilioni 63 kwa ajili ya miradi ya elimu zinazotokana na fedha za ahuweni ya
UVIKO-19.
Balozi
wa Korea ya Kusini Sun Pyo Kim, kwa upande wake alimuhakikishia Rais Dk. Mwinyi
kwamba Serikali ya Korea ya Kusini itaendelea kuiunga mkono Zanzibar katika
miradi yake mbali mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya elimu.
Balozi
Kim alitumia fursa hiyo kuipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa juhudi
zake za kuiimarisha sekta ya elimu.
Mapema
Mkurugenzi Mkaazi wa KOICA Kyucheol Eo
pamoja na Mkurugenzi Mkaazi wa ‘Good Neghbors’ kwa nyakati tofauti walieleza
hatua wanazozichukua katika kuiunga mkono Zanzibar kwenye sekta ya elimu huku
wakiahidi kuendeleza misaada yao ili kuhakikisha masomo ya Sayansi, Hisabati na
Kiingereza mafunzo yake yanatolewa kwa ufanisi mkubwa.
Wakati
huo huo, Rais Dk. Mwinyi alikabidhiwa vitabu vya miongozo ya mafunzo na
moduli kwa walimu pamoja na Kamati za
Skuli ambapo mapema mara baada ya kufika hoteli hapo alitembelea mabanda maalum
yaliyowekwa nyenzo za kufundishia na kupata maelezo juu ya namna za
kufundishia.
Imetayarishwa na Idara
ya Mawasiliano,
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment