Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi pia Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation ZMBF (kulia) akizungumza na Ujumbe wa Taasisi ya Rocke Feller unaoongozwa na Makamo wa Rais wa Taasisi hiyo Bw,Andrew Sweet(wa pili kulia) katika kusaidia na kuwezesha mfumo wa kutoa Chanjo ya Covid -19 kwa Wilaya ya Magharibi "A" na Kaskazini "A" Unguja,mazungumzo hayo yalifanyika leo katika Ofisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation ZMBF Migombani. [Picha na Ikulu] 25/10/2022.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi pia Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation ZMBF (kushoto) abadilishana mawazo na Makamo wa Rais wa Taasisi ya Rocke Feller Bw,Andrew Sweet mara baada ya leo mazungumzo yaliyofanyika leo katika Ofisi ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation ZMBF iliyopo Migombani Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja,mazungumzo hayo yaliyoashiria katika kuiwezesha na kusaidia mfumo wa kutoa Chanjo ya Covid -19 kwa Wilaya ya Magharibi "A" na Kaskazini "A" Unguja . [Picha na Ikulu] 25/10/2022
MKE wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi Mama Mariamu Mwinyi ameishukuru Jumuiya Health
Rockfeller Foundation kutoka nchini
Marekani kwa azma yake za kusaidia
juhudi za Serikali katika kujikinga na Ugonjwa wa Covid -19.
Mama Mariamu ambae pia ni Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) ametoa shukurani hizo
Ikulu Migombani mara baada ya mazungumzo
na Ujumbe wa Jumuiya Health Rockfeller Foundation ulioongozwa na Makamo wa Rais
Andrew Sweet, ambapo Jumuiya hiyo itasaidia Progamu ya utoaji wa chanjo za
Ugonjwa wa Covid-19 hapa nchini.
Amesema ZMBF inathamin juhudi za Jumuiya hiyo kwa vile
inayolenga kuimarisha afya za wananchi katika kujikinga na ugonjwa huo.
Alisema mradi huo ni wa mwaka mmoja
itatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Jumuiya hizo mbili , AMREF pamoja na
Wizara ya Afya katika Wilaya za Magharibi ‘A’ pamoja Kaskazini ‘A’ Unguja .
Nae, Makamo wa Rais wa Jumuiya ya Health Rockfeller Foundation
Andrew Sweet alisema ni jambo la faraja kwa Jumuiya hiyo kuwa na ushirikiano na
ZMBF na kupata fursa ya kuwasaidia huduma za chanjo ili wananchi waweze kukabiliana na ugonjwa Covid -19
Aidha, Mjumbe wa Bodi ya ZMBF Dk.
Ellen Mkondya Senkoro alisema Programu inayolengwa kutekelezwa ni kubwa na kubainisha matumaini yake kuwa mradi huo
utatowa matokeo chanya.
Imetayarishwa na Idaya ya Mawasiliano
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment