Habari za Punde

Wizara ya Elimu Yang'ara Michezo ya Riadha ya SHIMIWI Mkoani Tanga

Na Oscar Assenga,TANGA

TIMU ya Mchezo wa Riadhaa ya Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia imeng’ara katika Mashindano ya Shimiwi yanayoendelea Jijini Tanga huku wakimbiaji wake kuchukua nafasi za kwanza na pili katika mchezo uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Tanga Ufundi.

Wachezaji wa timu ya Elimu ilianza kwa kasi katika mchezo huo wa Riadhaa ambapo wakimbiaji wake walikuwa hari kubwa ya kukimbiza upepo ili kuweza kupata ushindi katika mashindano hayo.

Katika mchezo huo timu ya wanaume imefanya vizuri kwa upande wa mita 100 kupokezana vijiti huku kwenye zile za mita 200 wakiibuka washindi wa pili.

Kwa upande wa michezo mengine timu za Wizara hiyo walipambana mpaka kufikia hatua ya nane bora kwa mchezo wa kuvuta kamba ,mpira wa miguu,mpira wa pete .

Wakimbia Anitha Kihiyo kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia alishika nafasi ya pili nakikimbia mita 100 na Martine Zulumo  akichukua nafasi ya pili imekwenda Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na hivyo ametwaa media ya dhahabu.

Kwa upande wa riadhaa kupokeza vijiti wanaume nafasi ya kwanza imeenda kwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,

Akizungumza kuhusu mashindano hayo Makamu Mwenyekiti ywa timu ya Elimu Sports Deogratius Wenga alisema kwamba mashindano hayo yamekuwa na ushindani mkubwa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.