Habari za Punde

Serikali Kushirikiana na Wadau Kukabili Ugonjwa wa Kifuu Kikuu

 

Na Mwandishi wetu- Dodoma

Serikali imedhamiria kuendelea kushirikiana na wadau katika sekta zote ili kudhibiti na kutokomeza ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) ifikapo mwaka 2030.

Hayo yamesemwa na Katibu  Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi katika  kikao na Makatibu Wakuu wa Wizara kilichofanyika katika ofisi za Waziri Mkuu Jijini Dodoma.

“Ili kudhibiti ugonjwa huu wa Kifua Kikuu ni muhimu kushirikiana na wadau wengi kama sekta ya afya, wadau sekta ya elimu, sekta ya usafirishaji na sekta nyingine mbalimbali.” amesema Dkt. Yonazi.

Kwa upande wake Mtaalamu Mshauri kutoka Stop TB Partnership (STP) Bw. Oscar Mukasa wakati akiwasilisha taarifa ya mpango kazi wa kudhibiti Kifua Kikuu amesema watu wenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huo  ni pamoja na watu wanaoishi katika  makazi duni, Watoto, Wavuvi na  wanafunzi wanaoishi bweni.

“Kuna makundi mengine  ambayo yako hatarini kupata maambukizi Watu wenye VVU, watu wenye Utapiamlo, wachimbaji madini, wanaoishi na mgonjwa wa Kifua Kikuu, watoa huduma za afya na wanaotumia madawa ya kulevya kwa kujidunga sindano,” Ameeleza Mshauri huyo

Aidha Bw. Mukasa amewashauri wanaoishi katika mazingira hayo kuchukua tahadhari  za kujikinga na ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB).




Baadhi ya wajumbe wakifuatilia mada wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu kuhusu Kpango wa kisekta wa Kutokomeza Kifua kikuu Nchini.

Mkuu wa kitengo cha Tiba Kinga na Matunzo Mpango wa Taifa kifua kikuu na Ukoma kutoka Wizara ya Afya Dkt. Allan Tarimo akiwasilisha taarifa ya mpango kazi wa kudhibiti kipindupindu wakati wa kikao hicho.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (SBU) Dkt. Jim Yonazi akisaini Rasimu ya Mkakati wa Kisekta wa kuratibu uwajibikaji wa mapambano dhidi ya kifua kikuu Nchini.Kikao kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyuo Jijini Dodoma.

Na Mwandishi wetu- Dodoma

Serikali imedhamiria kuendelea kushirikiana na wadau katika sekta zote ili kudhibiti na kutokomeza ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) ifikapo mwaka 2030.

Hayo yamesemwa na Katibu  Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi katika  kikao na Makatibu Wakuu wa Wizara kilichofanyika katika ofisi za Waziri Mkuu Jijini Dodoma.

“Ili kudhibiti ugonjwa huu wa Kifua Kikuu ni muhimu kushirikiana na wadau wengi kama sekta ya afya, wadau sekta ya elimu, sekta ya usafirishaji na sekta nyingine mbalimbali.” amesema Dkt. Yonazi.

Kwa upande wake Mtaalamu Mshauri kutoka Stop TB Partnership (STP) Bw. Oscar Mukasa wakati akiwasilisha taarifa ya mpango kazi wa kudhibiti Kifua Kikuu amesema watu wenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huo  ni pamoja na watu wanaoishi katika  makazi duni, Watoto, Wavuvi na  wanafunzi wanaoishi bweni.

“Kuna makundi mengine  ambayo yako hatarini kupata maambukizi Watu wenye VVU, watu wenye Utapiamlo, wachimbaji madini, wanaoishi na mgonjwa wa Kifua Kikuu, watoa huduma za afya na wanaotumia madawa ya kulevya kwa kujidunga sindano,” Ameeleza Mshauri huyo

Aidha Bw. Mukasa amewashauri wanaoishi katika mazingira hayo kuchukua tahadhari  za kujikinga na ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB).

Baadhi ya Makatibu wa Wakuu na wawakilishi wa Makatibu Wakuu wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa kikao chao kilichohusu kuupitia na kuusaini Mpango wa Kisekta wa Kutokomeza Kifua Kikuu Nchini.

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.