Habari za Punde

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Philip Mpango Ametoa Mkono wa Pole kwa Familia ya Marehemu Edward Lowassa

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akiagana na Mbunge wa Monduli Mhe. Fredy Lowassa ambaye ni Mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu marehemu Edward Lowassa mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo na kuwafariji wafiwa katika makazi ya familia Masaki Jijini Dar es salaam

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango  akiweka Saini katika kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha  Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa wakati alipofika katika Makazi ya Familia Masaki Jijini Dar es salaam tarehe 11 Februari 2024. Kulia ni Mke wa Makamu wa Rais Mama Mbonimpaye Mpango.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango  akimfariji mjane wa  Waziri Mkuu Mstaafu marehemu Edward Lowassa ,Mama Regina Lowassa mara baada ya kuwasili nyumbani kwa familia hiyo Masaki Jijini Dar es salaam.
Mke wa Makamu wa Rais Mama Mbonimpaye Mpango akimfariji mjane wa Waziri Mkuu Mstaafu marehemu Edward Lowassa , Mama Regina Lowassa mara baada ya kuwasili nyumbani kwa familia hiyo Masaki Jijini Dar es salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango  akiwafariji waombolezaji mbalimbali wakati alipofika nyumbani kwa Waziri Mkuu Mstaafu marehemu Edward Lowassa Masaki Jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.