Bank of Africa Tanzania (BOA) imeeleza dhamira yake ya kuimarisha huduma zake zake zaidi kwendana na matakwa ya wateja sambamba na kuunga mkono jitihada za Serikali za kuwawezesha wanachi ili waweze kujipatia maendeleo sambamba na kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi.
Akiongea katika Iftar iliyoandaliwa na Benki hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Wasia Mushi, alisema benki hiyo itaboresha na kuendelea kukuza huduma zake za kibenki ikiwamo huduma za uwakala , simu na mifumo yote ya matumizi ya teknolojia (Tehama) katika jitihada za kukuza biashara na kuchochea ukuaji wa uchumi na kuwezesha makundi ya biashara ndogo na biashara za kati.
“benki yetu inatoa ahadi kuendelea kutoa huduma bora na uwajibikaji wa hali juu katika kuhakikisha ustawi wa wateja wetu na kuchochea maendeleo uchumi katika sekta mbalimbali hapa nchini,” aliongeza Bw Mushi
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji huyo alisema kuwa ni heshima kwa uongozi wa Benki kuandaa Iftar kwa wateja wa benki hiyo, pamoja na kukuza hisia za jumuiya kati ya imani mbalimbali.
Alisisitiza zaidi umuhimu wa kushiriki pamoja kupata Iftar katika mwezi mtukufu wa Ramadhani na umuhimu wa kuishi pamoja kidini na kuheshimiana kwa ajili ya kudumisha amani, maelewano na ustawi wa jamii.
Bank of Africa Tanzania (BOA) imeeleza dhamira yake ya kuimarisha huduma zake zake zaidi kwendana na matakwa ya wateja sambamba na kuunga mkono jitihada za Serikali za kuwawezesha wanachi ili waweze kujipatia maendeleo sambamba na kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi.
Akiongea katika Iftar iliyoandaliwa na Benki hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Wasia Mushi, alisema benki hiyo itaboresha na kuendelea kukuza huduma zake za kibenki ikiwamo huduma za uwakala , simu na mifumo yote ya matumizi ya teknolojia (Tehama) katika jitihada za kukuza biashara na kuchochea ukuaji wa uchumi na kuwezesha makundi ya biashara ndogo na biashara za kati.
“benki yetu inatoa ahadi kuendelea kutoa huduma bora na uwajibikaji wa hali juu katika kuhakikisha ustawi wa wateja wetu na kuchochea maendeleo uchumi katika sekta mbalimbali hapa nchini,” aliongeza Bw Mushi
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji huyo alisema kuwa ni heshima kwa uongozi wa Benki kuandaa Iftar kwa wateja wa benki hiyo, pamoja na kukuza hisia za jumuiya kati ya imani mbalimbali.
Alisisitiza zaidi umuhimu wa kushiriki pamoja kupata Iftar katika mwezi mtukufu wa Ramadhani na umuhimu wa kuishi pamoja kidini na kuheshimiana kwa ajili ya kudumisha amani, maelewano na ustawi wa jamii.
No comments:
Post a Comment