Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla ametoa agizo kwa uongozi wa Kampuni ya Lancet kuhakisha ndani ya mwezi mmoja kitengo cha wagonjwa walio katika uangalizi maalum (ICU) katika hospitali ya Wilaya ya Magharibi “B” Mwanakwerekwe Ijitimai kinatoa huduma ili kuondoa usumbufu wa ongezeko la wagonjwa katika hospital ya Rufaa ya Mnazi Mmoja.
Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea na
kukagua maendeleo ya utowaji na upatikanaji wa huduma za
Afya kwa wananchi katika hospital ya Wilaya ya Magharibi
“B” Mwanakwerekwe Ijitimai na Hospital ya Taifa ya Rufaa ya
Mnazi Mmoja Mkoa wa Mjini Magharibi.
Amesema kuwa Kampuni ya Lancet ina wajibu wa
kuhakikisha huduma zote muhimu zinapatika kwa ubora na
haraka kwa wagonjwa wanaofika katika hospitali zote za
Wilaya ili kuondosha msongamano wa wagonjwa katika
hospital za Rufaa ya Mnazi Mmoja.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Serikali ya
Awamu ya Nane imelipa kipaombele suala la kuboresha
miundombinu ya Afya ili kuzidi kutoa huduma bora za
kitabibu kwa Wananchi hivyo wananchi wanapaswa kuunga
mkono juhudi zinazochukuliwa na viongozi katika kuwaletea
maendeleo ikiwemo upatikanaji wa huduma bora za Afya.
Mhe. Hemed amewasisitiza madaktari kudumisha nidhamu
katika kazi kwa kufuata miiko, miongozo na maadili ya kazi
zao na kuachana na tabia ya kuwatolea lugha chafu wagonjwa
hasa wahuduma za Dharura ili kuendelea kuilinda heshima
ya wananchi ambapo Serikali haitamvumilia mtu yoyote
atakae kwenda kinyume na maadili ya kazi na itamchukulia
hatua za kisheria na kinidhamu kwa haraka .
Aidha Makamu wa Pili wa Rais amezitaka kampuni ya
Lancet na NSK zinazotoa huduma katika hospital za Wilaya na
Hospital ya Rufaa ya Mnazi Mmoja kuhakikisha changamoto
zote za vifaa, wataalamu na kiutendaji zinapatiwa ufumbuzi
kwa haraka ili kupunguza malalamiko kwa wananchi ambao
wameipa Imani Serikali yao ya kiwatumikia na kuwaletea
maendeleo.
Sambamba na hayo amewasisitiza wananchi kuendelea
kuzitumia Hospitali za Wilaya katika kutafuta matibabu
ambazo zinatoa huduma zote za kitabibu ili kupunguza wingi
wa wagonjwa katika hospitali za Rufaa.
Makamu wa Pili wa Rais amesema kuwa Serikali kuu
itahakikisha inatatua chamgamoto zote zinazoikabili Sekata
ya Afya zitapatiwa ufumbuzi wa haraka ili kuendelea kutoa
huduma bora na stahiki kwa wananchi bila ya ubaguzi wa aina
yoyote.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospital ya Rufaa
ya Mnazi Mmoja Dkt. Muhiddin Abdi Mahmoud amesema
katika kupunguza changamoto ya wataalamu katika
Hospitali za Wilaya na Rufaa Wizara ya Afya imeamua
kusomesha wafanyakazi wake kwa kuwalazimisha kusomea
zile kada ambazo zina upungufu wa madaktari ili kuweza
kutoa huduma zilizo bora na kwa wakati.
Amesema kuwa Wizara ya Afya imepanga kuandaa utaratibu
wa kuwashauri na kuwashawishi wanafunzi wanaojiunga na
vyuo vikuu kusomea kozi ambazo zina uhaba wa wataalamu
ikiwemo ICU, Ganzi na Usingizi pamoja na Huduma za
dharura ili kuweza kulisaidia Taifa kupata wataalamu wazawa.
Kwa upande wao wananchi waliofika hospitalini hapo kwa
ajili ya kupatiwa matibabu wameishukuru Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwajengea hospitali za Wilaya na
kuwasogezea huduma za matibabu karibu na makazi yao
zinazotoa huduma bora na kwa wakati sambamba na
kuwashukuru Madaktari kwa huduma bora wanazowapatia
wagonjwa wanaofika hospitalini hapo.
UHIDDIN ABDI MAHMOUD
amesema katika kupunguza changamoto ya wataalamu katika
Hospitali za Wilaya na Rufaa Wizara ya Afya imeamua
kusomesha wafanyakazi wake kwa kuwalazimisha kusomea
zile kada ambazo zina upungufu wa madaktari ili kuweza
kutoa huduma zilizo bora na kwa wakati.
Amesema kuwa Wizara ya Afya imepanga kuandaa utaratibu
wa kuwashauri na kuwashawishi wanafunzi wanaojiunga na
vyuo vikuu kusomea kozi ambazo zina uhaba wa wataalamu
ikiwemo ICU, Ganzi na Usingizi pamoja na Huduma za
dharura ili kuweza kulisaidia Taifa kupata wataalamu wazawa.
Kwa upande wao wananchi waliofika hospitalini hapo kwa
ajili ya kupatiwa matibabu wameishukuru Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwajengea hospitali za Wilaya na
kuwasogezea huduma za matibabu karibu na makazi yao
zinazotoa huduma bora na kwa wakati sambamba na
kuwashukuru Madaktari kwa huduma bora wanazowapatia
wagonjwa wanaofika hospitalini hapo.
No comments:
Post a Comment