Habari za Punde

Wachezaji wa Timu ya Simba SC.Watinga Ikulu Zanzibar Kumsalimia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk,Hussein Mwinyi

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhia Jezi ya Timu ya Simba na Nahodha wa Timu hiyo Mohammed Hussein, baada ya kumaliza mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Wachezaji wa Timu ya Simba na Viongozi wao, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 25-9-2024, wakiwa Zanzibar kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, dhidi ya Timu ya Azam unatakaofanyika katika uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar leo 26-9-2024.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisaini mpira kwa ajili ya kumbukumbu kwa Timu ya Simba, baada ya kumaliza mazungumzo na Wachezaji na Viongozi wa Timu hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
WACHEZAJI wa Timu ya Simba na Viongozi wao wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akizungumza na Wachezaji hao katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 25-9-2024, kwa ajili ya mazungumzo na kumsalimia, wakiwa Zanzibar kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Timu ya Azam utakaofanyika Uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar 26-9-2024
WACHEZAJI wa Timu ya Simba na Viongozi wao wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akizungumza na Wachezaji hao katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 25-9-2024, kwa ajili ya mazungumzo na kumsalimia, wakiwa Zanzibar kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Timu ya Azam utakaofanyika Uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar 26-9-2024
WACHEZAJI wa Timu ya Simba na Viongozi wao wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akizungumza na Wachezaji hao katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 25-9-2024, kwa ajili ya mazungumzo na kumsalimia, wakiwa Zanzibar kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Timu ya Azam utakaofanyika Uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar 26-9-2024.





SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema inajipanga kujenga uwanja mkubwa wa michezo utakaokuwa na vigezo vinavyokubalika na Shirikisho la Soka Duniani FIFA pamoja na Shirikisho la Soka Barani Afrika CAF.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipokutana na viongozi na wachezaji wa Klabu ya Simba ya Dar es Salaam waliofika kumsalimia kabla ya mchezo wao wa kesho dhidi ya Azam utakaochezwa Uwanja wa Amani Complex, majira ya saa mbili usiku.

Alisema, lengo la Serikali ni kuhakikisha michuano ya soka inayowashirikisha wachezaji wanaocheza ligi za ndani (Chan) na ile ya michuano ya soka ya mataifa ya Afrika kwa timu za taifa (AFCON), kuwa Zanzibar ni sehemu itakayochezwa michezo hiyo.

Amesema, Zanzibar imefanikiwa kwenye maeneo mbalimbali ya utalii ikiwemo utalii wa fukwe, urithi na makumbusho, hivyo wakati umefika sasa kwa Serikali na wadau wa utalii, kuangalia maeneo mengine ya kuutangaza utalii ikiwemo michezo.

Halikadhalika, alisema Serikali inaendelea kuwekeza na kuimarisha miundombinu ya michezo kwa kuendeleza ujenzi wa viwanja vya michezo vyenye hadhi ya kimataifa kwa maeneo yote ili michuano mikubwa ichezwe Zanzibar.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi ameelezea dhamira ya Simba ya kujenga kituo cha kuwaendeleza vijana katika mchezo wa soka hapa Zanzibar (soccer academy) kuwa ni jambo jema na kuwaahidi Serikali ipo tayari kuwaunga mkono kwa kuwapa eneo la ujenzi wa kituo hicho.

Pia, amevitaka vilabu vya michezo nchini kucheza michezo yao mingi Zanzibar ili kuimarisha sekta ya michezo pamoja kuinua mwamko wa vijana kupenda michezo.

Rais, Dk. Mwinyi amebainisha kuwa Zanzibar ina vipaji vingi vya vijana wanaohitaji kuendelezwa hususan kwenye mchezo wa soka ili kuwa na wachezaji wenye uwezo mkubwa wa kuzisaidia timu zao na timu za taifa.

Naye, Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu amemuhakikishia Rais Dk. Mwinyi kwamba Klabu hiyo ipo tayari kuitangaza Zanzibar kimataifa kupitia utalii wa michezo.

Vilevile, amepongeza juhudi za Rais Mwinyi kuendeleza viwanja vya michezo kila wilaya Unguja na Pemba, kwani michezo ni nyezo muhimu ya kukuza umoja, furaha na upendo miongoni mwa wananchi.

Simba Sports Club hivi karibuni ilifanikiwa kuingia hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika kwa kuitoa timu ya “Ahly Tripol” ya Libya na kuingia hatua ya makundi kwa mara ya saba.

IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.