Habari za Punde

MAKAMU WA RAIS AKIWASILI NCHINI ANGOLA DEC 04

  

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Angola Mhe. Balozi Téte António wakati akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Catumbela nchini Angola leo tarehe 04 Desemba 2024. Makamu wa Rais anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Marekani, Kongo na Zambia kuhusu Ushoroba wa Lobito (Lobito Corridor), ambapo Tanzania ni mgeni mwalikwa katika Mkutano huo unaofanyika katika mji wa Lobito nchini Angola tarehe 04 Desemba 2024.





No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.