Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akifanya
mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.
Balozi Thabiti Kombo mara baada ya kuwasili katika Mji wa Roma nchini Italia
tarehe 25 Aprili 2025. Makamu wa Rais anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwenye Mazishi ya
aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani hayati Baba Mtakatifu
Francisko yatayofanyika tarehe 26 Aprili 2025 Vatican.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na
Balozi wa Tanzania Vatican mwenye mkazi Berlin Mhe. Balozi Hassan Mwamweta
wakati akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Leonardo Da Vinci
uliopo Mjini Roma nchini Italia tarehe 25 Aprili 2025. Makamu wa Rais
anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Samia Suluhu Hassan, kwenye Mazishi ya aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Kanisa
Katoliki Duniani hayati Baba Mtakatifu Francisko yatayofanyika tarehe 26 Aprili
2025 Vatican.
No comments:
Post a Comment