Na
Kauthar Abdalla
KAMPUNI
ya JOVAGO imefungua inakusudua kuanzisha mipango ya kuweza kukodi hoteli ‘hotel
booking’, kwa wageni kupitia njia ya mtandao.
Akizungumza
na waandishi wa habari katika ukumbi wa ofisi ya umoja wa walemavu Zanzibar, ofisa
Uhusiano wa JOVAGO, Lilian Kisasa alisema kampuni hiyo itarahisisha upatikanaji
wa hoteli kwa njia ya mtandao popote alipo mgeni.
Kisasa
alisema huduma hiyo haitoshajihisha hoteli pekee bali pia itashajihisha kukuza
utalii kwa sababu itakuwa ni rahisi kwa mgeni anapokwenda sehemu kupata pahali
pa uhakika pa kukaa kwa ajili ya shughuli zake.
Aidha
alisema kwa sasa soko la mitandao liko wazi kutokana na mahitaji muhimu ya watu
ambayo wanatumia kila siku.
Pia
alisema kwa sasa kuna hoteli zaidi ya 1,000 Tanzania nzima ambazo wanazitumia
kuweka ‘booking’ kwa ajili ya wageni mbali mbali wanaokuja.
Hata
hivyo alisema soko la utalii litakuwa kubwa kwa sababu Tanzania nzima sehemu ambayo imeendelea kwa kuwa na
idadi kubwa ya vivutio ni Zanzibar ambapo pia kati ya hoteli zilizopo 160 zote
zipo Zanzibar.
Sambamba
na hayo alisema dunia imebadilika kiasi
ambacho wamiliki wa hoteli wanaangalia kukua kwa soko na utandawazi.
Alifahamisha
kuwa kampuni ya JOVAGO inalenga kuwafanya Watanzania waelewe utalii wa ndani
sio wageni pekee ambao wanaweza kuwa watalii ambapo kwa sasa amesema takwimu
zinaonesha kuwa kiwango cha kufanya boking kimepungua kutokana na harakati za
uchaguzi zilizopo nchini.
0 Comments