6/recent/ticker-posts

ZEC yafanya mdahalo kwa watu wenye ulemavu Pemba kuhusu uchaguzi

 MKALIMANI wa Lugha za alama kisiwani Pemba Asha Issa Mohamed, akiwatafsiria watu wenye ulemavu wa kusikia na kusema, katika mdahalo wa siku moja, ulioandaliwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kwa watu wenye Ulemavu kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MDHAMINI wa Tume ya Uchaguzi kisiwani Pemba, Ali Mohamed Dadi akizungumza na watu wenye ulamavu wa kusikia na kusema, katika mdahalo wa siku moja kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar kwa watu wenye ulemavu, mdahalo huo umefanyika Katika Skuli ya Madungu Chake Chake.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 AFISA Elimu kwa wapiga kura Tume ya Uchaguzi Zanzibar Juma Sanifu Sheha, akiwasilisha mada kwenye mdahalo wa siku moja kwa watu wenye Ulemavu wa kusinia na kusema, huko katika Ukumbi wa Madungu Sekondari Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 WATU wenye Ulemavu Kisiwani Pemba, wakiangalia mfano wa karatasi ya kupigia kura, wakati wa mdahalo wa siku moja kwa ulioandaliwa na tume ya Uchaguzi Zanzibar, huko katika skuli ya Madungu Sekondari Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MKALIMANI wa Lugha za alama kisiwani Pemba Asha Issa Mohamed akiwaonyesha watu wenye ulemavu wa kutokusema na kuzungumza mfano wa karatasi ya kupigia kuwa za urais wa Zanzibar, wakati wa mdahalo wa siku moja ulioandaliwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar, katika skuli ya Madungu Sekondari.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MSHIRIKI wa kongamano la watu wenyeulemavu kutoka Umoja wa watu wenyeulamavu Zanzibar ofisi ya Pemba, Hadija Mjaka akiuliza swali katika mdahalo wa siku moja ulioandaliwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar, katika skuli ya Madungu Sekondari.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
KAMISHNA wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Ayyoub Bakari akitoa ufafanuzi wa maswali ya watu wenye Ulemavu wa kutokusikia na kusema wakati wa mdahalo wa siku moja, katika skuli ya sekondari Madungu.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

Post a Comment

0 Comments