Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi (picha ya Maktaba) ametoa wito kwa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Ofisi zake kutekeleza kwa vitendo dhana ya uwazi na uwajibikaji kama yanavyozishinikiza Nchi Wanachama, kwa kile alichosema, utekelezaji wa dhana hiyo haupashwi kuwa ni jukumu la Serikali peke yake.Ametoa wito huo wakati wa majadilino ya Ripoti ya Baraza la Haki za Binadamu iliyowasilishwa mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa siku ya jumatatu
Na MwandishiMaalum, New York
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
imetoa wito kwa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, ikiwamo Baraza la Haki za Binadamu kuitekeleza kwa vitendo dhana ya uwazi na uwajibikaji.
Tanzania imesisitiza pia kwamba, haitoshi kwa Mashirika hayo kuzitaka nchi wanachama kwa maana ya serikali kuwajibika na kuwa wazi katika utekelezaji wa majukumu yake ili hali yenyewe yanafanya kinyume.
Wito huo umetolewa siku ya Jumatatu na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania katikaUmoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi, wakati Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, lilipokea na kujadili Ripoti ya Mwaka ya Baraza la
Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa.
Balozi Manongi ambaye alikuwa miongoni mwa Mabalozi kati ya wengi waliochangia Ripoti hiyo iliyowasilishwa na Rais wa Baraza
la Haki za Binadamu Bw .Joachim Rucker. Amesema, Tanzania
inatoa wito huo kutoka kile kinachoonekana dhahiri kwamba ama Mashirika hayo yamekuwa yakionyesha kuegemea upande mmoja dhidi ya mwingine au
kupendelea nchi moja dhidi ya nyingine kitendo ambacho kinakwenda kinyume na kile wanachokihubiri.
Akatoa mfano kwa kusema, wakati Rais wa Baraza la Haki za Binadamu akisisitiza katika ripoti yake umuhimu wa uwajibikaji,
Ofisi ya Haki za Binadamu katika mwezi Octoba ikishirikiana na UNICEF na
Canada, ilidhamini onyesho la
Filamu kuhusu kijana kutoka Geita mwenye alibinisim,
pasipo Taasisi hiyo kuujulisha Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania ili hali wakijua
Tanzania ilikuwa mlengwa wa filamu hiyo.
“Akiwasilisha Taarifa yake mbele ya Baraza hili mwanzoni mwa mkutao huu,
Rais wa Baraza la Haki za Binadamu amesisitiza umuhimu wa uwazi na uwajibikaji.
Cha kusikitisha tukio la
konyeshwa kwa filamu ambayo maudhui yake yalihusu Tanzania na sisi kama Tanzania
hatukujulishwa, hakika inakwenda kinyume kabisa na dhana ambayo Rais wa Baraza la Haki za Binadamu amekizungumza hapa” akasema Balozi Manongi
Na kuongeza“ ndiyo maana Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania inatoa wito kwa Mashirika ya Umoja wa Mataifa au Ofisi zake kuonyesha kwa vitendo dhana ya uwazi, uwajibikaji na kutoegemea upande wowote”.
Akabainisha kuwa, Mashirika ya Umoja wa Mataifa hayapashwi kujionyesha kuwa yanaegemea upande wowote
au hata kupendelea baadhi ya nchi wanachama dhidi nchi nyingine na hasa pale ambapo Mashirika hayo binafsi hayajapitia na kujiridhisha juu ya kile ambacho wanataka kukiunga mkono au
kutaka kujihusisha nacho.
Akaeleza Zaidi
mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwamba, Tanzania
haikupinga na wala haipingi filamu kuhusu kijana wa Geita,
filamu iliyolenga katika kuonyesha changamoto zinazowakabili watu wenye ualibino nchini
Tanzania
“
Tulichopinga na tunachopinga ni maelezo yaliyoandikwa na muandaaji wa filamu hiyo, maelezo ambayo yalikuwa na upotoshaji mkubwa.
Kwa mfano,baadhi ya maelezo ya filamu hiyo yanasema, hakuna utashi wa kisiasa kutoka Serikali ya
Tanzania
katika kukabili uovu wanaotendewa watu wenye ualibino. Kwamba,
msukumo kutoka mataifa ya nje ni walazima ili kutokomeza uovu huo, kwamba ujinga ni laana kubwa inayowakabili waaafrika na jawabu pekee ni kuwaelimisha,
kwamba filamu hiyo ilikuwa ni kuwashawishi watu wanje ili kuleta mabadiliko ya kweli.
Na vile vile filamu hiyo ilikuwa ni kusherehekea roho ya
utu na kazi nzuri inayofanywa na watu wa Canada katika kuwasaidia watu wenye ualibino” akasisitiza Balozi Manongi
Akasema Balozi, Ni
kwa kuzingatia upotoshaji huo na mwingine ulioelezwa na muandaaji wa filamu hiyo,
haishangazi kuona kwamba Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania haukualikwa kufadhili onyesho la
filamu hiyo iliyoonyeshwa Umoja wa Mataifa.
“ Rais wa Baraza la Haki za Binadamu pia
amezungumzia wajibu wa Asasi za Kijamii katika uhamasishaji wa haki za Binadamu. Tunakubaliana na pendekezo wake.
Wakati tunauga mkono mchango wa Asasi za kijamii,
nilazima basi Asasi hizo nazo zikaonyesha uwajibikaji na uwazi pamoja na kujipambanua katika utekelezaji wa majukumu yao.
Uwajibikaji hauwezi kuwa ni jukumu la serikali peke yake” akasisitiza Balozi Manongi.
Akizungumzia Zaidi
kuhusu changamoto zinazowakabili watu wenye ualibino, Mwakilishi huyo wa Tanzania,
amesema, Tanzania kwa kutambua changamoto kubwa za kijamii na kiuchumi pamoja na upatikanaji wa haki za msingi kwa watu wenye ualibino ndiyo maana kwa kushirikiana na Malawi
imeamua kuwasilisha mbele ya Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Azimio kuhusu watu wenye ualibino.
Amesema dhumuni kuu la Azimio hilo na ambalo linatarajiwa kupitishwa
wiki hii ni kupanua wigo na ushiriki mpana wa wadau mbali mbali ukiwamo Umoja wa Mataifa katika kuzikabili changamaoto zinazowakabili watu wenye ualibino.
Na kwa sababu hiyo,
Balozi Manongi ameziomba nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa,
kuunga mkono azimio hilo pamoja na jitihada zinazofanywa na Serikali ya Tanzania
pamoja na Chama cha Watu wenye Ualibino
Tanzania (TAS) katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili watu wenye ualibino vikiwamo vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa na watu wasio na mapenzi mema.

0 Comments