6/recent/ticker-posts

BOT YAAGIZWA KUONGEZA UDHIBITI WA MIKOPO UMIZA

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Deogratius Luswetula (Mb) akiiagiza Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuendelea kuongeza udhibiti wa mikopo yenye riba kubwa (mikopo umiza) wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Mhe. Dkt. Neema Peter Majule, aliyetaka kufahamu Serikali imechukua hatua gani kwa watu ambao wamejinufaisha kwa mikopo yenye riba kubwa, bungeni jijini Dodoma.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, 

Wizara ya Fedha)

Na. Peter Haule, WF, Dodoma.


Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Deogratius Luswetula 


(Mb) ameiagiza Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuendelea 


kuongeza udhibiti wa mikopo yenye riba kubwa (mikopo 


umiza) ili wananchi wapate mikopo yenye tija.

 


Ametoa maagizo hayo  bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu 


swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Mhe. Dkt. 


Neema Peter Majule, aliyetaka kufahamu hatua 


zilizochukuliwa na Serikali kwa watu wanaojinufaisha kwa 


kutoza riba kubwa kwenye mikopo, hatua inayopunguza 


jitihada za Serikali za kuwakwamua wananchi kiuchumi 


hususani wanawake na vijana.

 

Mhe. Luswetula alisema kuwa Serikali imeanza kuchukua 


hatua kwa wote wanaokiuka taratibu zilizowekwa na Serikali 


za utoaji mikopo kwa kusitisha leseni zao na hatua nyingine za 


kisheria.

 

“Wizara ya Fedha imejipanga kuhakikisha taasisi zote 


zinazotoa mikopo zinafuata taratibu na tayari Serikali 


imeandaa rasimu ya kusimamia mikopo ya kidigitali 


inayotarajiwa kuanza kutekelezwa Mwaka wa Fedha 


2026/2027”, alisema Mhe. Luswetula.

 

Akijibu swali la msingi kuhusu hatua zilizochukuliwa kudhibiti 


mikopo hatarishi inayotolewa na baadhi ya taasisi zisizo 


rasmi, Mhe. Luswetula alisema kuwa Serikali, BoT na wadau 


wengine, imechukua hatua mbalimbali za kudhibiti mikopo 


hatarishi yenye riba kubwa kwa kuendelea kutoa elimu kwa 


wananchi.

 

Alisema kuwa mikopo inapaswa kutolewa na watoa huduma 


wenye leseni kutoka BoT kwa mujibu wa Sheria ya Benki na 


Taasisi za Fedha ya Mwaka, 2006 pamoja na Sheria ya 


Huduma Ndogo za Fedha ya Mwaka, 2018.

 

Hatua nyingine iliyochukuliwa ni pamoja na kuwatambua na 


kuchukua hatua za kiutawala dhidi ya watoa mikopo 


wasioidhinishwa ambapo programu 69 za mikopo ya kidigitali 


zilizobainika kutoa mikopo bila leseni zilisitishwa na 


programu 126 zilifungiwa.

 

Vilevile kutoa Mwongozo maalum kwa watoa huduma za 


mikopo ya kidigitali ili kuhakikisha uwazi, uendeshaji wa 


kimaadili, utoaji wa taarifa kamili kuhusu gharama za mikopo 


pamoja na ulinzi wa watumiaji wa huduma za kifedha.

 

Mhe. Luswetula alilitaja eneo lingine kuwa ni pamoja na 

kuandaa rasimu ya kanuni za kusimamia mikopo ya kidigitali, 

ambazo zinatarajiwa kuanza mwaka wa fedha 2026/27 

ambapo Kanuni hizo zinalenga kuimarisha udhibiti wa 

wakopeshaji wa kidijitali nchini Tanzania.

 

Aidha, Mhe. Luswetula alisema kuwa Serikali kupitia Wizara 


ya Fedha, imekuja na programu ya elimu ya fedha ya mwaka 


2020/2021 hadi 2025/2026 ikiwa ni mpango maalum wa 


kutoa elimu kwa wananchi kwa makundi yote ambayo 


inalenga kuwawezesha wananchi kupata uelewa, maarifa na 


kuwajengea maarifa ya kusimamia mapato na matumizi na 


kufanya maamuzi sahihi katika kutumia huduma rasmi za 


kifedha.


Alisema kuwa Wizara ya Fedha kila mwaka 


imekuwa ikiadhimisha Wiki ya Huduma ya Fedha Kitaifa 


kuanzia mwaka 2021 na mwaka huu yamefanyika Jijini Tanga 


kuanzia Januari 21, lengo likiwa wananchi kupata elimu ya 


fedha.

 

Mhe. Luswetula alisema miongoni mwa Mikoa ambayo 


maadhimisho hayo yamefanyika kuanzia mwaka 2021 ni 


pamoja na Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya na sasa 


Tanga.

 

Hadi sasa takribani mikoa 16 imefikiwa na huduma ya elimu 


ya Fedha na zaidi ya wananchi 64,000 wamefikiwa ikiwa ni 


pamoja na wanawake 40,000 na wanaume 24,000 na  


Halmashauri 94.

 

Mwisho.

 

Post a Comment

0 Comments