6/recent/ticker-posts

THBUB yafika kijiji cha Dunga kuwapa elimu ya haki za binadamu.

Naibu Sheha wa Shehia ya Dunga Kiembeni, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, Bw. Kesi Makame Mussa akiwakaribisha wanashehia wa kijiji hicho (hawapo pichani) katika mkutano wa pamoja baina yao na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) Februari 17, 2026.

Afisa Uchunguzi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, THBUB ofisi ya Zanzibar, Bw. Abdullatif Ali Sheha (kushoto aliyesimama) akiwasilisha mada ya “Haki za Binadamu na Misingi ya Utawala Bora” kwa wananchi wa kijiji cha Dunga Kiembaeni, Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja, Februari 17, 2026.


Afisa Sheria, Wilfred Msagati akiwasilisha mada ya “majukumu ya THBUB” katika mkutano wa pamoja baina ya Tume hiyo na wananchi wa Shehia ya Dunga Kiembeni, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, Februari 17, 2026,

THBUB yafika kijiji cha Dunga kuwapa elimu ya haki za binadamu.

NA MWASHAMBA JUMA, (THBUB)

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, THBUB ofisi ya Zanzibar, imewajengea uelewa mpana wanakijiji wa Dunga Kiembeni kuhusu masuala ya uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora.

Akizungumza na wanakijiji hao kwenye mkutano wa pamoja baina ya Tume na wananchi wa Shehia ya Dunga Kiembeni iliopo Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, Afisa Sheria wa THBUB Bw. Wilfred Msagati aliwahimiza wananchi hao kutambua haki zao na kuzipambania pale zinapovunjwa.

Sambamba na kuwaelekeza kufika Tume kwa lengo la kuwasilisha malalamiko yao endapo watakupamba na masuala ya uvunjwaji wa haki na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora.

Wilfred aliyasema hayo wakati akiwasilisha mada ya “Majukumu ya THBUB” kwa wanajijiji hao pamoja ya kuwaelimisha haki mbalimbali ambazo binaadamu zinamstahikia na kumuwajibikia huku akiwafahamisha jinsi ya Tanzania ilivyoridhia mikataba ya kimataifa kutekeleza haki za binadamu zikiwemo haki za watoto, haki za watu wenye mahitaji maalumu wakiwemo wazee na watu wenye ulemavu.

Aidha, aliwaeleza wanakijiji hao, mbali na majukumu mengi yanayotekelezwa na THBIUB pia Tume hiyo ina jukumu la kuhamasisha nchini hifadhi ya haki za binadamu, wajibu kwa jamii na kueneza nchini elimu kwa umma kuhusu haki za binadamu na utawala bora.

Katika mkutano huo pia, Wilfred aliwaeleza wanakijiji hao jukumu la THBUB kutembelea maeneo mbalimbali ambayo watu huzuiliwa kwa lengo la kutoa elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora, vikiwemo vyuo vya mafunzo na magereza, maeneo yanayohifadhiwa wazee kwa lengo la kutunzwa na vituo vya kulelea watoto yatima.

Naye, Afisa Uchunguzi wa THBUB ofisi ya Zanzibar, Bw. Abdullatif Ali Sheha wakati akiwasilisha mada ya “Haki za Binadamu na Misingi ya Utawala Bora” kwa wananchi wa kijiji hicho, amesema lengo la mkutano huo ni kuwajengea uelewa wnanchi hao ili watambue masuala ya uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora.

Pia Bw. Abdul aliwahimiza wananchi hao kufika Tume kwa lengo la kuwasilisha malalamiko yao pamoja na kuwaelewesha jinsi ya kuwasilisha mamalamiko hayo Tume ili  yapatiwe ufumbuzi.

Kwa upande wa wanchi hao, waliishukuru THBUB na kuipongeza kwa jitihada zao za kuwafikia wananchi wa vijijini pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili.

Jumla ya malalamiko manne ya wanakijiji cha Dunga Kiembeni yalipokelewa katika mkutano huo yakiwemo matatu ya uvunjifu wa haki za binadamu na lalamiko moja lilihusu ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Aidha, wananchi wengine waliahidi kufika Tume kuwasilisha malalamiko yao.


Post a Comment

0 Comments