Ameyasema hayo wakati wa mashindano ya kuhifadhi Qur-ani yaliyoandaliwa na Al-Madrasatul Wakfiyatul Islamiya huko Kwa alinatu, Wilaya ya Mjini.
Amesema kuwa mashindano hayo ni njia muhimu ya kuwahamasisha watoto kujifunza na kuipenda Qur-ani, sambamba na kuwajengea msingi mzuri wa maisha yao ya baadaye.
Aidha amewapongeza walimu na waandaaji wa mashindano hayo kwa jambo zuri walilolifanya kwa juhudi kubwa ya kuwahifadhisha Qur ani wanafunzi wa chuo hicho yatayosaidia kukulia katika maadili mema ya kiislamu
Akisisitiza Jamii kuendeleza kusoma qur ani Kwa wingi Katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani mwezi ambao umeshuka Qur-an ambayo ni uongofu kwa waumini
Amefahamisha kwamba Katika mambo matatu muhimu ya kuyatekeleza ni kutoa sadakatul jaria, kupata elimu yenye manufaa ambayo ukawafundisha na wengine pamoja na kuwa na mtoto mwema ambaye atakuombea dua .
Nao Waandaaji wa mashindano hayo wamesema lengo la kuandaa mashindano hayo ni kuwahamasisha watoto kujifunza, kuhifadhi na kuzingatia mafundisho ya Qur-ani katika maisha yao ya kila siku ili iweze kuyafaa duniani na akhera .
Kwa Upande wa Sheha wa Shehia ya Kwaalinatu Salmini Shaabani Mzee amesema amepata faraja kuona katika Shehia hiyo kuzalishwa vipaji vya kuhifadi Qur-ani na kuwashukuru walioandaa jambo hilo.
Mashindano hayo yamewakutanisha wanafunzi kutoka madrasa mbalimbali ambapo washindi walipatiwa zawadi mbalimbali pamoja na pesa taslim kama ishara ya kutambua juhudi zao katika kuhifadhi Qur-an
mashindano ya kuhifadhi Qur-ani yaliyoandaliwa na Al-Madrasatul Wakfiyatul Islamiya yakifadhiliwa na Vikosi cha Valentia Zanzibar 'KVZ' pamoja na Tropical Air.
Imetolewa na Kitengo cha Habari .
WHSUM.



.jpg)

0 Comments