Habari za Punde

L & B Hospital Kufunguliwa June 4

 Hii ndiyo Hospitali Mpya ya L&B iliyopo eneo la Chukwani karibu na kituo cha mwisho cha Daladala na Jirani na Chuo Kikuu cha Chukwani. Inafunguliwa rasmi tarehe 4 June 2012 na itatoa huduma za out patient pamoja na huduma zote za uzazi - Maternity Wing
L&B ina lengo la kutoa huduma anazostahiki mgonjwa kupewa kama mgonjwa kwa mujibu wa hali yake na kujali maslahi yake (Value for Money). Iko chini ya Daktari bingwa wa mambo ya uzazi Gynacologist Dk Otta J Lymo na Dk Hakim Bilal ambaye kwa sasa ndiye mkuu wa Chuo cha Afya Mbweni.

Kwa mahitaji yote ya afya pamoja na mambo ya uzazi mnakaribishwa L&B Hospital Chukwani.

1 comment:

  1. Kila la kheri, ila wajitahidi kuboresha huduma wasije wakageuka Al Rahma walianza vizuri baadae wamekua bora M/ladu.

    Tena cha kujiuliza wenzetu, wanashindwa nini wakati matibabu ni bashara? Watu wanafika India, A. kusini na Bara kutafuta matibabu na mote humo wanalipa pesa za usafiri,malazi na matibabu.

    Naamini matibabu yakiwa karibu hata kama ni ghali kidogo watu watajitahidi.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.