Habari za Punde

Zanzibar Kuanzisha Mfuko wa Bima ya Afya


Na Khadija Khamis –Maelezo Zanzibar      13/7/2012 .

Serikali ya Zanzibar inatarajia kuanzisha mfuko wa  bima ya afya ili kuweza kuwaondolea usumbufu wa tiba wananchi wake .

Hayo yamesemwa  katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi na Naibu Waziri wa Afya, Dk. Sira Ubwa Mamboya wakati akijibu suala la Jaku Hashim Ayoub  Mwakilishi wa Jimbo  la  Muyuni  aliyetaka kujua uanzishwaji  mfuko wa bima ya  afya  kwa Zanzibar.

Dk. Sira alisema kwamba uanzishwaji wa huduma ya bima ya afya kwa Zanzibar ni tayari na hivi sasa iko katika hatua za awali za kufanya tafiti za kuweza kujua utayari  wa uwezo wa wananchi .


Alisema kuwa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya imeshawapatia mafunzo wafanyakazi wa Wizara ya afya Zanzibar juu ya jinsi ya kuendeleza mfuko huo kwa hospitali zote za serikali Binafsi na NGO kwa  unguja na Pemba .

Dk. Sira alisema mfuko wa bima ya afya ya Zanzibar umeshafungua ofisi yake na kuweza kuwajiri wafanyakazi wake wakiwemo daktari, muhasibu, na dereva .

Aidha alisema kuwa tumaini ni kwamba mfuko huo utafanyakazi vizuri kwa lengo la kuziwezesha hospitali za Serikali za Unguja na Pemba ziweze kunufaika na huduma hiyo.

Akieleza dhamana ya uazishwaji wa mfuko huo alisema itasimamiwa na Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Kwa upande wa mfuko wa bima wa taifa,alisema tayari umeanza kufanya kazi zake Zanzibar kuanzia mwaka 2007 na una jumla ya wanachama 5,393 ukichanganya pamoja na familia zao idadi  inafikia 28,044 wanafaidika na mfuko huo.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.