6/recent/ticker-posts

Wahanga wa moto Tumbe wafarijiwa

Na Salama Salim Pemba.
 Katika kuwafariji wahanga wa waliofikwa na janga la moto katika maeneo tofauti ya kijiji cha Tumbe wilaya ya Micheweni Mkoa wa kaskazini Pemba ,wametakiwa kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu kilichowakumba miongoni mwao.
 
Hayo yameelezwa jana na Makamo Mwenyekiti wa Halmashauri wa Wilaya ya Micheweni, Kombo Hassan Khamis kwa niaba ya Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Abdalla Ali Said wakati alipokuwa akizungumza na wahanga wa ajali hiyo huko kijijini kwao.
 
Alisema kuwa kutokana na janga la moto huo ulioingia katika kijiji cha Tumbe mashariki umekuwa ni wakushangaza sana hali ambayo imeleta mfadhaiko mkubwa wakaazi wanaoishi maeneo hayo.
 
Alifahamisha kuwa kutokana na janga hilo halmashauri ya wilaya ya micheweni itachukuwa hatuwa za maksudi kwa ajili ya kuwasaidia wale wote ambao wamepatwa na janga hilo .
 
“kutokana na janga hili la kushangaza kwa wahanga hawa halmashauri hii haina budi kuchukuwa hatuwa za makusudi kwa ajili ya kuwasaidia wale wote ambao wameathirika”,alifahamisha Mwenyekiti huyo.
 
Nae Sheha wa shehia ya Tumbe Mashariki Seif  Omar Juma alisema nivyema kwa kwa halmashauri hiyo kuwaangalia kwa jicho la imani wahanga hao.
 
Alisema kuwa kwa kipindi hichi mfuko wa kamati ya maendeleo ya jimbo la Tumbe ni mdogo sana kwa hivyo wachukuwe hatua za makusudi za kutoa msaada kwa waathirika waliopatwa na janga hilo .
 
“Tunaiomba halmashauri hii kwa hali na mali kuweza kutoa mchango wao ili kuweza kutusaidia kwa hawa walioathirika waliofikwa na janga hili kutokana na mfuko wetu wa jimbo ni mdogo kwa sasa”,alisema sheha huyo.
 
Hata hivyo alisema halmashauri hiyo hainabudi kuweza kutoa mchango wao kwa lengo la kuwasaidia katika shughuli za ujenzi kwa wahanga hao.
 
Sambamba na hayo alioa wito kwa serikali na wasamaria wema kuweza kutoa misaada mbali mbali kwa lengo la kuwahami wale wote waliofikwa na janga hilo .
 

Post a Comment

0 Comments