Na Masanja Mabula, Pemba
MTOTO wa kike, mkaazi wa kijiji cha Tondooni Makangale Pemba amelazwa katika hospitali ya Chake Chake kisiwani Pemba kwa matibabu baada ya kujiripua kwa moto.
Habari zilizopatikana kutoka kijijini kwao zinasema mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa kidatu cha pili (jina tunamuhifadhi) alipatwa na mkasa huo baada ya kugombwa na mama yake mzazi.
Tukio hilo linadaiwa kutokea usiku wa manane kuamkia jana Jumapili Novemba 25.
Mwanafunzi huyo kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Chake Chake Pemba, akipatiwa matibabu na hali yake inasemekana kuwa bado mbaya kutokana na kuungua vibaya maeneo takriban yote ya mwili wake.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Saleh Mohammed, alisema kuwa chanzo cha tukio hilo, ni mtoto huyo kukutwa akiwa na mtoto wa kiume.
Kaimu Kamanda huyo aliwataka Wazazi kutumia lugha nzuri wanapozungumza na watoto wao ili kuwaepusha kuchukua ghadhabu za ghafla ambazo hatimae hazitomuathiri yeye peke yake bali na familia nzima.
Alifahamisha kuwa mtoto huyo baada ya kugombwa na mama yake ndipo alipoamua kuchukua uamuzi huo mbaya ambapo majirani ndio waliofanikiwa kuokoa maisha yake kwa kumwagia maji.
Habari zaidi za tukio hilo zinatarajiwa kutolewa na madaktari ambao kwa sasa wanahangaikia hali yake inayotajwa kuwa ni mbaya.
REA Yagawa Majiko na Mitungi ya Gesi kwa Watumishi wa Magereza Kagera
Kuunga Mkono Matumizi ya Nishati Safi
-
Na Diana Byera, Bukoba
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamezindua zoezi la kugawa majiko na
mitungi ya gesi 486 kwa watumishi wote wa magereza nane za m...
26 minutes ago
No comments:
Post a Comment