Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amemteuwa Dkt Abdullah Ismail Kanduru kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Cha Sayansi za Afya ,Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa iliotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dkt Abdulhamid Yahya mzee amesema kuwa Rais amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa kifungu cha 7(1) cha Sheria ya Chuo cha Sayansi za Afya,Zanzibar namba 10 ya mwaka 1998.
Uteuzi huo umeanza leo.
NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment