Na Madina Issa
SERIKALI
ya Mapinduzi ya Zanzibar na serikali ya Uholanzi
zimetiliana saini mkataba wa mradi wa kuimarisha afya ya mama wajawazito
na watoto katika hospitali kuu ya
Mnazimmoja pamoja na hospitali za wilaya 21 Unguja na Pemba.
Utiaji
saini msaada huo ulifanyika katika ofisi ya Wizara ya Fedha, Uchumi na Mipango
ya Maendeleo ambapo kwa upande wa Zanzibar iliwakilishwa na Katibu Mku wizara hiyo, Khamis Mussa Omar na
Balozi wa Uholanzi nchini Dk. Ad Koekkoek aliiwakilisha nchi yake.
Katika
mkataba huo, Uholanzi itaipatia Zanzibar
shilingi bilioni 19.2 kutekeleza mradi huo.
Katibu
Mkuu Mussa, alisema msaada huo unakwenda sambamba na kusaidia utekelezaji wa Mkakati
wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar
(MKUZA II) pamoja na malengo ya maendeleo ya milenia.
Alisema
msaada huo unalenga kusaidia uimarishaji huduma za mama na watoto Zanzibar na inajumuisha
utanuzi wa majengo ya hospitali kuu ya Mnazimmoja utakaohusisha jengo
lililokusudiwa kuwa kiwanda cha dawa liliopo karibu na hospitalI hiyo.
Aidha alisema
pia utashughulikia ujenzi wodi mpya ya wazazi, idara ya kupokelea wagonjwa wa
kawaida na waliopata ajali pamoja na kutanua wodi ya wazazi na watoto zilizopo
sasa.
Maeneo
mengine yatakayonufaika ni kuimarisha, kutengeneza na kujenga hospitali za 21
za wilaya na kuwekwa vifaa muhimu
vitakavyowezesha kutoa huduma bora kwa mama na watoto.
Mradi
huo utatekelezwa katika kipindi cha miaka minane.
No comments:
Post a Comment