Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Dadi Faki
Dadi, akizungumza na Wahanga waliofikwa na mtihani wa kuunguliwa moto Majumba
yao huko katika kiwanja cha Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Pemba, kabla
ya kupokea msaada ya kutoka ZSTC.
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Dadi Faki
Dadi, akipokea Msaada wa Chakula kwa niaba ya Wahanga waliounguliwa moto huko
Shehia ya Shumba mjini na Maziwa ng’ombe Wilaya ya Micheweni, kutoka kwa
Uongozi wa ZSTC Zanzibar,ukiongozwa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika hilo,
Mwanahija Almas Ali , huko Micheweni Pemba.
Mkurugenzi Mwendeshaji wa ZSTC Zanzibar,
Mwanahija Almas Ali, akizungumza na Wahanga hao huko katika Viwanja vya Ofisi
ya Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Pemba.
Nyumba ambazo tayari zinaendelea kujengwa
huko katika Shehia ya Maziwa Ng’ombe huko Micheweni ambazo zinajengwa na
Wananchi wenyewe kufuatia kuunguwa kwa moto.
Mkurugenzi Mwendeshaji wa ZSTC, Zanzibar,
Mwanahija Almas Ali, akiangalia Nyumba zinazojengwa kufuatia Mtihani huo wa
kuunguwa moto huko katika Shehia ya Maziwa Ng’ombe Pemba.
Mkurugenzi Mwezeshaji wa ZSTC Zanzibar
,Mwanahija Almas Ali, akipokea Maelezo juu ya moto ulivyotokezea kutoka kwa
Wanakamati ya Maafa ya Shehia ya Maziwa Ng’ombe na jinsi wanavyoendeleza Ujenzi
wa Nyumba hizo.
Picha na Bakar Mussa –Zanzibarleo –Pemba.
No comments:
Post a Comment