Habari za Punde

Mihangaiko ya ununuzi wa futari Pemba

 
BAADHI ya wafanya Biashara ya ndizi za aina mbali mbali, wakiwa katika mnada wa ndizi ndani ya soko kongwe la chake chake, ambapo bei ya bidhaa hizo katika mwezi huu wa Ramadhani zimepanda bei kupitia kiasi, mkungu mmoja uliokuwa ukiuza kati ya 8000 hadi 10000 upanda kufikia elfu 20000 hadi 30000.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 
KUFUATIA mwezi Mtukufu wa Ramadhani kufika, bidhaa ya ndizi mbivu aina ya mkono mmoja, zimepanda bei maradufu kidole kimoja kilichokuwa kikiuzwa shilingi 500 hadio 700 na kupanda hadi kufikia 1500 na 2000.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

 
BIASHARA ya ndizi imeonekana kupendwa na wananchi wengi katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani, pichani mteja akinunua ndizi ya mkono mmoja katika soko la chake chake.(Picha na Bakari Mussa,PEMBA.)

~~
MFANYABIASHARA wa ndizi katika soko la Chake Chake, akimuuzia mtenja ndizi aina ya mkono mmoja, kama alivyokutwa na mpiga picha wetu.(Picha na Wapiga Picha wetu, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.