Gavana wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Katika Benki ya Maendeleo ya Afrika,Dkt. Servicus B.Likwelile ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali akiteta jambo na Mawaziri wa Fedha mbalimbali waliohudhuria mkutano huo Mjini Abijah-Ivory coast.
Baadhi
ya Marais wa Afrika waliohudhuria mkutano wa maadhimisho ya miaka 50 ya Benki
ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Mjini Abijah-Ivory coast.
Rais
wa Benki wa Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Donald Kaberuka akiwa kwenye kikao
na Magavana wa Afrika wakijadiliana changamoto mbalimbali za maendeleo
zilizojitoketeza katika nchi za Afrika Mjini Abijah- Ivory coast.
Gavana wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Katika Benki ya Maendeleo ya Afrika, ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servicus B.Likwelile akiwa na ujumbe kutoka Tanzania waliohudhuria mkutano wa majadiliano pamoja na Mkurugenzi Mkuu Bw. Gabrriel Negatu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Abijah-Ivory coast
Gavana wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Katika Benki ya Maendeleo ya Afrika, Dkt. Servicus B.Likwelile ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji akitoa ufafanuzi kwa Kamishna wa Fedha za Nje Bw. Ngosha Magonya akiwa pamoja na Afisa Mwandamizi Bw. John L. Sima Mjini Abijah-Ivory Coast.
Rais
Mpya wa Benki ya Maendeleo ya Afrika(AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina akihutubia na
kutoa shukrani kwa wajumbe kwa kuchanguliwa kuwa rais wa benki hiyo Mjini
Abidjan-Ivory Coast.
Rais
Mpya wa Benki wa Maendeleo ya Afrika(AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina akiwa pamoja
na baadhi ya marais kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB) Mjini
Abidjan-Ivory Coast.(Picha zote na Scola Malinga-Abidjan).
Maelezo hayaendani na picha..Gavana Ndullu hayupo pichani kama unavyoeleza!
ReplyDelete